Sunday, 29 September 2013

MPANDA FM RADIO

kwa habari motomoto na za uhakika skiliza Mpanda Radio 97.0 FM na tembelea blog yao "www.mpandaradio.blogsports.com"

Saturday, 28 September 2013

MATOKEO LIGI KUU ENGLAND



by rahim kassonga

SPURS, CHELSEA SARE, TORRES KADI NYEKUNDU!
AVB, MOURINHO WAPEANA MIKONO!
RATIBA/MATOKEO:
BPL: LIGI KUU ENGLAND
Jumamosi 28 Septemba

Tottenham Hotspur 1 Chelsea 1
Tottenham wametoka Sare Bao 1-1 na Chelsea na kuipiku Arsenal
 kileleni mwa Ligi Kuu England lakini Arsenal ambao wanacheza hii leo Ugenini wanaweza kurudi kileleni wakitoka Sare na Swansea City.
Gylfi Sigurdsson ndie alieifungia Spurs Bao katika Kipindi cha Kwanza baada ya ushirikiano mzuri kati ya Christian Eriksen na Roberto Soldado na Mpira kumfikia yeye.

MAGOLI:
Tottenham 1 - 0 Chelsea
Sigurdsson Dakika ya 19
Tottenham 1 - 1 Chelsea
Terry Dakika ya 65

Chelsea walimwingiza Juan Mata mara Kipindi cha Pili kilipoanza na frikiki yake ndio iliunganishwa na John Terry kwa kichwa na kusawazisha Bao.

Juan Mata alisaidia sana kubadilisha hali ya mchezo na kuingia kwake hakukuisaidia Chelsea kurudisha goli tu, bali pia kushambulia zaidi na kutaka kupata goli la ushindi

pengine kocha wa Chelsea leo atakuwa ameona uwezo na mchango wa Mata nakuanza kumwanzisha kwenye mechi zijazo

matokeo mengine  



 Fulham 1-0 Cardiff City


17:00 Hull City v West Ham United
17:00 Manchester United v West Bromwich Albion
17:00 Southampton v Crystal Palace
19:30 Swansea City v Arsenal
++++++++++++++++++++++++++++

++++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
NA
TIMU
MECHI
PTS
1
Tottenham
6
13
2
Arsenal
5
12
3
Chelsea
6
11
4
Man. City
5
10
5
Liverpool
5
10
6
Everton
5
9
++++++++++++++++++++++++++++
Chelsea walimaliza Mechi wakiwa Mtu 10 baada ya Fernando Torres kupewa Kadi ya Njano ya pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu zikiwa zimebaki Dakika 10 Mpira kwisha.
Sare hii imewafanya Chelsea wakamate Nafasi ya 3.
Kivutio cha Mechi hii kilikuwa mzozo kati ya Andre Villas-Boas na Jose Mourinho, Watu ambao wanatoka Nchi moja Ureno na walifanya kazi pamoja kwa Miaka 7, waliporushiana maneno lakini kabla ya Mechi kuanza walipeana mikono na mwisho wa Mechi kukumbatiana.
VIKOSI:
Spurs: Lloris, Walker, Dawson, Vertonghen, Naughton, Paulinho, Dembele, Townsend, Eriksen, Sigurdsson, Soldado
Akiba: Chiriches, Lamela, Holtby, Defoe, Chadli, Friedel, Sandro.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Luiz, Terry, Cole, Ramires, Mikel, Lampard, Oscar, Torres, Hazard
Akiba: Essien, Mata, Schurrle, Schwarzer, Cahill, Azpilicueta, Eto'o.
Refa: Mike Dean
++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
BPL: LIGI KUU ENGLAND
Jumapili 29 Septemba
15:30 Stoke City v Norwich City
18:00 Sunderland v Liverpool
Jumatatu 30 Septemba
22:00 Everton v Newcastle United  
++++++++++++++++++++++++++++

RONALDINHO KAUMIA, KULIKOSA KOMBE LA DUNIA KWA VILABU



by rahim kassonga
KOMBE LA DUNIA KWA KLABU:


NI MOROCCO 2013: DESEMBA 11 HADI 21!
STAA MKONGWE wa Klabu ya Brazil Atletico Mineiro, Ronaldinho, amechanika Musuli ya
gaucho
kwenye Nyonga na sasa yuko hatarini kuyakosa Mashindano makubwa ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu yatakayochezwa huko Morocco kuanzia Desemba 11.
Atletico Mineiro ndio Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini CONMEBOL baada ya kutwaa Copa Libertadores.
Mashindano hayo yataanza kuchezwa huko Morocco kuanzia Desemba 11 hadi 21 na kushirikisha Klabu Bingwa za kila Bara pamoja na Raja Casablanca ya Morocco ambayo imeingizwa kama Mwenyeji.


WASHIRIKI:
FIFA KOMBE LA DUNIA KWA KLABU:
Zinaanza Nusu Fainali:
-Brazil Atlético Mineiro [Brazil] Bingwa CONMEBOL
-Bayern Munich [Germany] Bingwa
Zinaanza Robo Fainali:
-Bingwa Asia HAJAJULIKANA
-Bingwa Afrika HAJAJULIKANA
-Monterrey [Mexico] Bingwa CONCACAF
Zinaanza Mchujo kabla kuingia Robo Fainali:
-Auckland City [New Zealand] Bingwa OFC
-Raja Casablanca [Morocco] Mwenyeji

Daktari wa Atletico Mineiro Rodrigo Lasmar amesema maumivu ya Ronaldinho, ambae amewahi kuzichezea Klabu za Ulaya, AC Milan na Barcelona, yanaweza kuchukua hadi Miezi mitatu kupona lakini wameshaanza kumtibu kwa bidii.

Wednesday, 25 September 2013

THEO WALCOTT KUFANYIWA UPASUAJI

by rahim kassonga


FOWADI wa Arsenal Theo Walcott atakuwa nje ya Uwanja kwa Wiki kadhaa kwani Jumatano anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa Tumbo huko Ujerumani ili kutibu matatizo ya majeruhi aliyopata kwa ndani.
Akithibitisha habari hizi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekiri kuwa Walcott atakuwa nje kwa Wiki kadhaa.

Matatizo haya yatamfanya Mchezaji huyo azikose Mechi mbili muhimu za mwisho za England za kuwania kufuzu kwenda Brazil Mwakani kwenye Fainali za Kombe la Dunia ambazo wanatakiwa washinde ili wajihakikishie kufuzu.
England watacheza na Montenegro Hapo Oktoba 11 na kumalizia Mechi ya mwisho ya Kundi lake na Poland hapo Oktoba 15 na Mechi zote hizo zitachezwa Wembley Jijini London.
Walcoot alishawahi kupata matatizo ya aina hii Mwezi Machi na kuwa nje ya Uwanja kwa Wiki 3.
Hata hivyo, Wenger amehakikisha kuwa tatizo la Walcott sio kubwa sana na muda mfupi baada ya Operesheni yake ataanza tena Mazoezi mepesi.