Sunday, 29 September 2013
MPANDA FM RADIO
kwa habari motomoto na za uhakika skiliza Mpanda Radio 97.0 FM na tembelea blog yao "www.mpandaradio.blogsports.com"
Saturday, 28 September 2013
MATOKEO LIGI KUU ENGLAND
by rahim kassonga
SPURS,
CHELSEA SARE, TORRES KADI NYEKUNDU!
AVB,
MOURINHO WAPEANA MIKONO!
RATIBA/MATOKEO:
BPL:
LIGI KUU ENGLAND
Jumamosi
28 Septemba
Tottenham
Hotspur 1 Chelsea 1
Tottenham
wametoka Sare Bao 1-1 na Chelsea na kuipiku Arsenal
kileleni mwa Ligi Kuu
England lakini
Arsenal ambao wanacheza hii leo Ugenini wanaweza kurudi kileleni wakitoka Sare
na Swansea City.
Gylfi
Sigurdsson ndie alieifungia Spurs Bao katika Kipindi cha Kwanza baada ya
ushirikiano mzuri kati ya Christian Eriksen na Roberto Soldado na Mpira
kumfikia yeye.
MAGOLI:
Tottenham
1 - 0 Chelsea
Sigurdsson
Dakika ya 19
Tottenham
1 - 1 Chelsea
Terry
Dakika ya 65
Chelsea
walimwingiza Juan Mata mara Kipindi cha Pili kilipoanza na frikiki yake ndio
iliunganishwa na John Terry kwa kichwa na kusawazisha Bao.
Juan Mata alisaidia sana kubadilisha hali ya mchezo na kuingia kwake hakukuisaidia Chelsea kurudisha goli tu, bali pia kushambulia zaidi na kutaka kupata goli la ushindi
pengine kocha wa Chelsea leo atakuwa ameona uwezo na mchango wa Mata nakuanza kumwanzisha kwenye mechi zijazo
matokeo mengine
Fulham 1-0 Cardiff City
17:00
Hull City v West Ham United
17:00
Manchester United v West Bromwich Albion
17:00
Southampton v Crystal Palace
19:30
Swansea City v Arsenal
++++++++++++++++++++++++++++
++++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
|
NA
|
TIMU
|
MECHI
|
PTS
|
|
1
|
Tottenham
|
6
|
13
|
|
2
|
Arsenal
|
5
|
12
|
|
3
|
Chelsea
|
6
|
11
|
|
4
|
Man.
City
|
5
|
10
|
|
5
|
Liverpool
|
5
|
10
|
|
6
|
Everton
|
5
|
9
|
++++++++++++++++++++++++++++
Chelsea
walimaliza Mechi wakiwa Mtu 10 baada ya Fernando Torres kupewa Kadi ya Njano ya
pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu zikiwa zimebaki Dakika 10 Mpira kwisha.
Sare
hii imewafanya Chelsea wakamate Nafasi ya 3.
Kivutio
cha Mechi hii kilikuwa mzozo kati ya Andre Villas-Boas na Jose Mourinho, Watu
ambao wanatoka Nchi moja Ureno na walifanya kazi pamoja kwa Miaka 7,
waliporushiana maneno lakini kabla ya Mechi kuanza walipeana mikono na mwisho
wa Mechi kukumbatiana.
VIKOSI:
Spurs: Lloris, Walker, Dawson, Vertonghen, Naughton, Paulinho,
Dembele, Townsend, Eriksen, Sigurdsson, Soldado
Akiba:
Chiriches, Lamela, Holtby, Defoe, Chadli, Friedel, Sandro.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Luiz, Terry, Cole, Ramires, Mikel, Lampard,
Oscar, Torres, Hazard
Akiba:
Essien, Mata, Schurrle, Schwarzer, Cahill, Azpilicueta, Eto'o.
Refa: Mike Dean
++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
BPL:
LIGI KUU ENGLAND
Jumapili
29 Septemba
15:30
Stoke City v Norwich City
18:00
Sunderland v Liverpool
Jumatatu
30 Septemba
22:00
Everton v Newcastle United
++++++++++++++++++++++++++++
RONALDINHO KAUMIA, KULIKOSA KOMBE LA DUNIA KWA VILABU
by rahim kassonga
KOMBE
LA DUNIA KWA KLABU:
NI
MOROCCO 2013: DESEMBA 11 HADI 21!
STAA
MKONGWE wa Klabu ya Brazil Atletico Mineiro, Ronaldinho, amechanika Musuli ya
| gaucho |
kwenye Nyonga
na sasa yuko hatarini kuyakosa Mashindano makubwa ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa
Klabu yatakayochezwa huko Morocco kuanzia Desemba 11.
Atletico
Mineiro ndio Mabingwa wa Nchi za Marekani ya Kusini CONMEBOL baada ya kutwaa
Copa Libertadores.
Mashindano
hayo yataanza kuchezwa huko Morocco kuanzia Desemba 11 hadi 21 na kushirikisha
Klabu Bingwa za kila Bara pamoja na Raja Casablanca ya Morocco ambayo
imeingizwa kama Mwenyeji.
WASHIRIKI:
FIFA
KOMBE LA DUNIA KWA KLABU:
Zinaanza
Nusu Fainali:
-Brazil
Atlético Mineiro [Brazil] Bingwa CONMEBOL
-Bayern
Munich [Germany] Bingwa
Zinaanza
Robo Fainali:
-Bingwa
Asia HAJAJULIKANA
-Bingwa
Afrika HAJAJULIKANA
-Monterrey
[Mexico] Bingwa CONCACAF
Zinaanza
Mchujo kabla kuingia Robo Fainali:
-Auckland
City [New Zealand] Bingwa OFC
-Raja
Casablanca [Morocco] Mwenyeji
Daktari
wa Atletico Mineiro Rodrigo Lasmar amesema maumivu ya Ronaldinho, ambae amewahi
kuzichezea Klabu za Ulaya, AC Milan na Barcelona, yanaweza kuchukua hadi Miezi
mitatu kupona lakini wameshaanza kumtibu kwa bidii.
Wednesday, 25 September 2013
THEO WALCOTT KUFANYIWA UPASUAJI
by rahim kassonga
FOWADI
wa Arsenal Theo Walcott atakuwa nje ya Uwanja kwa Wiki kadhaa kwani Jumatano
anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa Tumbo huko Ujerumani ili kutibu matatizo ya
majeruhi aliyopata kwa ndani.
Akithibitisha
habari hizi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekiri kuwa Walcott atakuwa nje
kwa Wiki kadhaa.
Matatizo
haya yatamfanya Mchezaji huyo azikose Mechi mbili muhimu za mwisho za England
za kuwania kufuzu kwenda Brazil Mwakani kwenye Fainali za Kombe la Dunia ambazo
wanatakiwa washinde ili wajihakikishie kufuzu.
England
watacheza na Montenegro Hapo Oktoba 11 na kumalizia Mechi ya mwisho ya Kundi
lake na Poland hapo Oktoba 15 na Mechi zote hizo zitachezwa Wembley Jijini
London.
Walcoot
alishawahi kupata matatizo ya aina hii Mwezi Machi na kuwa nje ya Uwanja kwa
Wiki 3.
Hata
hivyo, Wenger amehakikisha kuwa tatizo la Walcott sio kubwa sana na muda mfupi
baada ya Operesheni yake ataanza tena Mazoezi mepesi.
Subscribe to:
Posts (Atom)