Tuesday, 24 September 2013

MSIMAMO| LIGI KUU BARA

by rahim kassonga

MSIMAMO, RATIBA, MATOKEO LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA



NA
TIMU
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Simba SC
5
3
2
0
13
4
9
11
2
JKT Ruvu
5
3
0
2
6
2
4
9
3
Coastal Union
5
2
3
0
5
2
3
9
4
Ruvu Shooting
5
3
0
2
6
3
3
9
5
Azam FC
5
2
3
0
8
6
2
9
6
Kagera Sugar
5
2
2
1
6
3
3
8
7
Mbeya City
5
1
4
0
5
4
1
7
8
Yanga SC
5
1
3
1
10
7
3
6
9
Mtibwa Sugar
5
1
3
1
3
4
-1
6
10
Rhino Rangers
5
0
4
1
5
7
-2
4
11
JKT Oljoro
5
1
1
3
3
6
-3
4
12
Mgambo JKT
5
1
1
3
2
10
-8
4
13
Tanzania Prisons
5
0
3
2
3
9
-6
3
14
Ashanti United
5
0
1
4
2
11
-9
1

Print or Email this page
Description: Print
WAFUNGAJI WA MABAO LIGI KUU 2013
JINA TIMU MABAO
Amisi Tambwe Simba SC 6
Jerry Tegete Yanga SC 3
Haruna Chanongo Simba SC 3
D. Kavumbangu Yanga SC 3
Jonas Mkude Simba SC 2
Elias Maguri Ruvu Shoot 2
Bakari Kondo JKT Ruvu 2
Paul Nonga Mbeya City 2
Saad Kipanga Rhino 2
Kipre Tchetche Azam FC 2
Themi Felix Kagera 2

EDITOR:TIDA SAIDEA

TANZANIA YATWAA UBINGWA AIRTEL RISING STARS WANAWAKE, YATOA PIA WACHEZAJI BORA

by rahim kassonga



TIMU ya wasichana ya Tanzania imeibuka mabigwa katika michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya kimataifa ya Airtel Rising Stars yaliyokuwa yanafanyika mwaka huu nchini Nigeria, baada ya kuifunga Kenya bao 1-0 katika Fainali. 

mabingwa kwa wanawake






Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania kwa kufunga bao hilo pekee la ushindi jana.
Tanzania ilikua kundi moja na Sierra-Leone, Malawi, na Uganda. Walishinda mechi moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1, wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda na kutoka sare na Malawi 1-1.



Katika Robo Fainali, mabinti wa kibongo wakashinda 4-2 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya DRC Uwanja wa NIS Sports, kabla ya kuifumua Uganda kwa mabai 8-1 kwenye Nusu Fainali.
Mbali na ushindi huo wa wasichana wa Tanzania walijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji bora wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora kwa upande wa wasichana Shelda Boniface.
Kwa upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya Airtel Rising Stars ilifanyika kweny uwanja wa Agege nchini Nigeria.










Niger wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu katika mechi sita. Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda.
Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo
Michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, National Institute for Sports Fiels na Main Bowl.
Mashindano ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanafanyika kwa mara ya pili mwaka huu na yamekua bora kwa vijana wadogo na kwa kuzingatia jinsia.

TANZANIA YATWAA UBINGWA AIRTEL RISING STARS WANAWAKE, YATOA PIA WACHEZAJI BORA

by rahim kassonga



TIMU ya wasichana ya Tanzania imeibuka mabigwa katika michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya kimataifa ya Airtel Rising Stars yaliyokuwa yanafanyika mwaka huu nchini Nigeria, baada ya kuifunga Kenya bao 1-0 katika Fainali. 




Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania kwa kufunga bao hilo pekee la ushindi jana.
Tanzania ilikua kundi moja na Sierra-Leone, Malawi, na Uganda. Walishinda mechi moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1, wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda na kutoka sare na Malawi 1-1.



Katika Robo Fainali, mabinti wa kibongo wakashinda 4-2 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya DRC Uwanja wa NIS Sports, kabla ya kuifumua Uganda kwa mabai 8-1 kwenye Nusu Fainali.
Mbali na ushindi huo wa wasichana wa Tanzania walijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji bora wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora kwa upande wa wasichana Shelda Boniface.
Kwa upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya Airtel Rising Stars ilifanyika kweny uwanja wa Agege nchini Nigeria.










Niger wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu katika mechi sita. Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda.
Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo
Michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, National Institute for Sports Fiels na Main Bowl.
Mashindano ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanafanyika kwa mara ya pili mwaka huu na yamekua bora kwa vijana wadogo na kwa kuzingatia jinsia.

MARIO BALOTELLI:-‘LUPANGO KWA ‘KUMTISHA REFA!!!!’

by rahim kassonga


Mario Balotelli amefungiwa Mechi 3 kwa kutumia ‘vitisho na matusi’ dhidi ya Refa mara baada ya Mechi ya Serie A Juzi ambayo Timu yake AC Milan ilichapwa Bao 2-1 na Napoli Uwanja wa kwao San Siro.
Balotelli alitolewa kwa Kadi Nyekundu baada ya Mechi hiyo kwisha kufuatia kupewa Kadi ya Njano ya Pili baada ya yeye kuvaana na Mchezaji wa Napoli Valon Behrami na kisha kuanza kukwaruzana na Refa Luca Banti.
Katika Mechi hiyo, Balotelli alikosa Penati iliyookolewa na Kipa wa Napoli, Pepe Reina, na baadae kupiga shuti lililogonga mwamba na Dakika za mwisho kuifungia AC Milan hilo Bao lao moja kwa Shuti murua.
Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kabisa kwa Balotelli kukosa Penati tangu aanze Soka la Kulipwa.
AC Milan haijasema lolote kama itakata Rufaa kupinga Kifungo hicho na kama kitabaki kama kilivyo basi Balotelli atazikosa Mechi za Serie A dhidi ya Bologna, Sampdoria na Juventus.
Wakati huon huo, Wasimamizi wa Soka huko Italy wameamuru AC Milan kufunga Jukwaa lao la Uwanja wa San Siro linaloitwa Curva Sud kwenye Mechi ijayo na Sampdoria kama Adhabu kwa Mashabiki waliokuwa wakighani Kibaguzi wakati wa Mechi waliyofungwa na Napoli.

Chadema wamtangazia vita Dk Mathayo David



by rahim kassonga
KILIMANJARO
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza operesheni maalumu ya kumuondoa Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi Dk David Mathayo David katika Uchanguzi Mkuu wa 2015.
Operesheni hiyo imepewa jina la Operesheni Mathayo Out kwa kifupi (OMO) imeanza wiki iliyopita kwa kufanya Mikutano ya hadhara Jimboni humo na itaendelea tena wiki ijayo.
Aidha Mmoja wa Makamanda wa Operesheni hiyo Gervas Mgonja amesema kuwa Jimbo hilo limekuwa chini ya himaya ya CCM tangu Uhuru lakini wananchi wake wapo kama wamefunga ndoa na tatizo la maji.
Dk Mathayo ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi alipoulizwa kuhusu operesheni hiyo ya kumuondoa madarakani amesema kuwa Chadema ni chama kidogo na hakimnyi usingizi kwa madai uwezo wa kampeni unaishia Himo.


EDITOR:TIDA SAIDEA