Friday, 25 October 2013

MAJANGA KWENYE ELIMU, WANAFUNZI 471, MADAWATI 39, MADARASA 4, WAPI SERIKALIII !!!!!

by rahim kassonga (La Captain)


Shule ya msingi Ilebula iliyopo Kata ya Kabungu Wilaya ya Mpanda vijijini wametoa changamoto wanazo kabiliananazo katika mazingira ya shule ikiwemo upungufu wa madarasa,madawati na nyumba za walimu.

Akiongea na Mpanda Fm Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Moses Mathias Makalawa amesema kuwa shule hiyo ina upungufu wa vyumba vya madarasa ambapo shule nzima ina madarasa manne hali inayopelekea wanafunzi kusomea chini ya mti na wengine katika ofisi za walimu.

Makalawa ameongeza kuwa shule hiyo ina wanafunzi 471 ambapo madawati katika shule nzima ni 39 ambayo hayakidhi idadi ya wanafunzi na kupelekea wengine kukaa chini huku walimu wakiishi mbali na mahali pa kazi kutokana na shule hiyo kumiliki nyumba mbili za walimu.

Hata hivyo  mwalimu Makalawa ametoa wito kwa serikali kutatua changamoto hizo ili kuongeza ufaulu katika shule hiyo na kufanikisha mpango wa Big Result Now ulioanzishwa na serikali.




NANDO APEWA NAFASI YA KIPEKEE KUSHIRIKI TENA BIG BROTHER AFRICA YA MWAKANI 2014.

by zangii ze icon After being disqualified from the recently concluded BBA The Chase show, Nando Khan (also known as Ammy Nando) has gotten himself another chance at the game!


Word reaching us right now is that, he will be representing Tanzania in the 9th season of the Big Brother Africa show, tagged BBA Stars.

Reliable sources also reveal that he has accepted the offer and will be back in the house come next year.

The Tanzania rep got disqualified shortly after his fight with Ghana's Elikem.

Nando is rumored to have apologized to Elikem during the finale party.

Msanii wa bongo movie anusurika kuliwa KIBOGA.....Alizidisha pombe na kujikuta chooni akiwa mtupu.





Muigizaji wa filamu za kibongo anayejulikana kwa jina la Danny Cloud  maarufu  kama  Danny mtoto wa mama  ambaye  alipata  umaarufu  wa  jina  hilo  kupitia  filamu ya mtoto wa mama  amenusurika  kubakwa ( kuliwa kiboga ) 

Akizungumza  na  mpanda fm, rafiki wa karibu wa msanii huyo  alidai kwamba  Danny  alikuwa maeneo ya Bilcanas  ambapo  alipewa  ofa  ya  pombe  na  jamaa  zake...

Rafiki huyo  alidai  kuwa, baada  ya  kupewa  ofa  hiyo  adimu, msanii  huyo  alianza  kuiparamia  pombe mfano  wa  mtu  mwenye  kiu  kali  ya  maji, hali  iliyomfanya  asijitambue  na  kuanza  kuvua  nguo...

"Kuna  wakati Danny  alinyanyuka  na  kuelea  chooni  huku  akipepesuka...Alipofika  huko  alidondoka  na kulala  huko huko chooni, hali  iliyowafanya   vibaka  watake  kumla  kiboga"...Alisema  huyo rafiki  yake  na  kuongeza:

"Baada  ya  kimya  kirefu, ilibidi  tukamwangalie  ambapo  tuliwakurupusha  vijana  watatu  wakiwa  wameshamvua  nguo"

MAZISHI YA NYAISANGAH... MAMIA WAMLILIA CHALZ HILLARY


by zangii ze icon
Stori: Waandishi Wetu
VILIO vilitawala juzi Jumanne wakati nguli katika utangazaji Bongo, Julius Nyaisangah ‘Uncle J’ akiagwa, lakini wengi walionekana kumlilia zaidi swahiba wake wa karibu, Charles Hillary ‘Chalz Hillary’.
Jopo la waandishi wetu lililofika mapema katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar katika Ibada ya kumuaga marehemu, lilishuhudia mijadala ikiendelea katika makundi kuhusu upweke alioachwa nao Hillary.
Kwa sasa Hillary ni mtangazaji katika Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) lenye makao yake makuu, jijini London.
 
Charles Hillary ‘Chalz Hillary’.
Mwandishi mmoja mwandamizi aliyekataa jina lake kutajwa, alisikika akisema; “Nilimsikia Charles Hillary akihojiwa BBC, alilia sana, akasema lazima aje amzike rafiki yake, lakini mpaka sasa sijamuona. Masikini, kama namuona vile, atakuwa na hali mbaya.”
Mwingine alisema: “Inawezekana amechelewa ndege lakini kama atafanikiwa kuja, anaweza kukodisha ndege ndogo ikamuwahisha  Tarime kwenye mazishi, maana anazikwa

HESHIMA
Watangazaji na wadau wa habari nchini waliofika viwanjani hapo waliipongeza serikali kwa heshima kubwa waliyompa marehemu Nyaisangah kwa kuomba shughuli za kuagwa kwa mwili wake ifanyike pia Dar es Salaam, ambako alikuwa na marafiki wengi.

Mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais, Dk. Ali Gharib Bilal ambaye alitoa salamu zake za rambirambi na kuwataka wanafamilia na wanahabari wote kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu.
VINGOZI WENGINE
Mbali na Dk. Bilal, vingozi wengine waliohudhuria shughuli hiyo ni pamoja na Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa taifa we Chadema, Freeman Mbowe, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa na viongozi wengine.

Mbali na hao, Mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari (MOAT) Dk. Reginald Mengi, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, John Kitime ambaye aliwawakisha wanamuziki wote na Mkurugenzi wa Aset, Asha Baraka.
WATANGAZAJI 
Ukiacha waandishi wa habari wa magazeti mbalimbali waliohudhuria, pia walikuwepo watangazaji wengi wa kizazi cha sasa na wale waliowahi kufanya kazi na marehemu Radio Tanzania Dar es Salaa (RTD – sasa TBC Taifa) na Radio One.
Baadhi yao ni pamoja na Rainfred Masako, Mikidadi Mahamud, Enock Ngombare Mwiru, Misanya Bingi, Masoud Masoud, Abdallah Mwaipaya, Betty Mkwasa, Godwin Gondwe, Issac Gamba, Allan Lawa na Abdallah Majura.
SAFARI YA TARIME
Baada ya shughuli ya kumuaga Uncle J, taratibu nyingine ziliendelea ambapo alitarajiwa kusafirishwa kwa ndege ya kukodi kwenda Tarime, Mara kwa maziko yaliyopangwa kufanyika juzi Jumatano.

Thursday, 24 October 2013

MAMA KANUMBA ATAKA MCHUNGAJI AKAMATWE


by zangii ze icon
Stori: zangii koroboy
SIKU chache baada ya mchungaji aliyejitambulisha kwa jina moja la Mayanga kuibuka na kudai ndiye amewaua Steven Kanumba na Hussein Mkiety ‘Sharo Milionea’, mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa ametaka jamaa huyo akamatwe mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda kuwa ndiye aliyewaua Steven Kanumba na Hussein Mkiety ‘Sharo Milionea’.
Mbali na kudai kumuua Kanumba na Sharo, Mchungaji Mayanga alidai kabla ya kuokoka kuwa alihusika na vifo vya watu milioni 605 wakiwemo wasanii wa Kundi la Five Stars wapatao 14 na mwanamuziki James Dandu ‘Mtoto wa Dandu’ kwa njia za kichawi.
Mara baada ya gazeti la Amani toleo namba 782 la Oktoba 17, mwaka huu kuripoti habari hiyo, mama Kanumba alipelekewa nakala yake nyumbani ambapo baada ya kuisoma, ndipo alipoona kuna kila sababu ya mchungaji huyo kukamatwa kwa kuwa atakuwa amehusika moja kwa moja na kifo cha mwanaye Kanumba. “Mama Kanumba alipata mshtuko mkubwa siku ile alipoliona lile gazeti, maskini alikuwa tayari ameanza kusahau machungu ya kuondokewa na mwanaye,” kilisema chanzo kilicho karibu na mama Kanumba.
Mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa.
Mara baada ya chanzo hicho kupenyeza habari hizo, paparazi wetu alimtafuta mama Kanumba ili kumuuliza alipokeaje habari za mchungaji huyo ambapo alipopatikana, alitiririka; “Naiomba serikali imkamate huyo mchungaji, maana yeye si amesema amemuua mwanangu, sasa iweje aendelee kutanua mtaani wakati ameweka wazi kuwa amemuua mwanangu. “Imeniuma sana, ameamsha machungu ambayo tayari nilianza kuyasahau. Huyo mchungaji akamatwe na sheria imchukulie hatua stahiki,” alisema mama Kanumba.
 
Marehemu Steven Kanumba.
Hata hivyo, katika ushuhuda alioutoa mchungaji huyo, alijitabiria kuwa ipo siku atakamatwa na kufungwa kutokana na siri za vigogo ambao aliwapa utajiri kwa nguvu za giza. “Nina siri za watu wengi sana, nikiwaambia mtaogopa na nchi itatikisika. Najua siku moja watu watanikamata na kunifunga pingu kwa siri nilizonazo, lakini kamwe siogopi kwa kuwa Bwana ameniongoza,” alisema.
Juzi gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta mama Sharo Milionea, Zainabu Mkiete lakini hakupatikana kwani simu yake iliita bila ya kupokelewa. Mchungaji huyo alipotafutwa naye simu yake iliita bila kupokelewa.

SOMA HABARI YA MCHUNGAJI ALIYEDAI KUWAUA SHARO, KANUMBA: HAPA

JOKATE: DIAMOND ALITAKA TUZAE


by zangii zen icon
Stori: Mwandishi Wetu
MTANGAZAJI maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amefunguka kuwa aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ alitaka wazae kipindi walipokuwa wapenzi.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Jokate alifunguka hayo juzikati alipokuwa akifanya mahojiano maalum na mapaparazi , pamoja na kufunguka mengi, alibainisha kuwa Diamond huwa anapenda watoto kwenye uhusiano.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
“Mh! Diamond anapenda kuzaa, tena siyo kwangu tu wanawake wake wote huwa nasikia anataka kuzaa nao,” alisema Jokate.

WATANZANIA WANUSURIKA KIKAANGONI TUSKER PROJECT FAME


WASHIRIKI wanaowakilisha nchi ya Tanzania katika mashindano ya Tusker Project Fame msimu wa sita yanayofanyika nchini Kenya wamenusurika kuingia kikaongoni wiki hii.

Washiriki hao walionusurika kuingia katika kikaango hicho ni Hisia, pamoja na Angel, ambapo wameonesha hali ya matumaini ya kuendelea kuwepo na kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Washiriki walioingia katika kingao hiko ni pamoja na Fess (kenya), Jennifer (Kenya),  Mishel (Kenya)Undercover Brother (Uganda), hali inayoonesha hati hati ya washiriki wa nchi ya Kenya.

Akielezea sababu ya washiriki hao kuingia katika kikaangoni 'Probation' jaji mwenye machachari Ian Mbugua alieleza kuwa shindano hilo halitafuti wasanii wa kawaida bali wenye vipaji na uwezo mkubwa zaidi Afrika Mashariki.

"Kwao hiyo  ni changamoto kuingia ndani ya probation mashindano haya hatutafuti wasanii wa kawaida tu ,bali tunatafuta wasanii wenye uwezo mkubwa, hivyo ili kujitoa kikaangoni lazima waongeze juhudi" alisema Ian

Wema Sepetu atumia milioni 13 kuibadili ngozi yake akiwa China baada ya kuharibiwa sana na Mkorogo


IMEVUJA! Kumbe ile safari ya nchini China ya Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu ‘Madam’ lengo lilikuwa kubadili ngozi ya mwili wake katika mwonekano mpya ambayo ilishaharibika kwa mkorogo.
 
Wema Sepetu ‘Madam’.
 
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, staa huyo aliingia nchini humo na mdogo wake aitwaye Bite ambaye kazi yake kubwa ilikuwa kufanya mawasiliano na nyumbani, Tanzania endapo lingetokea baya wakati wa zoezi hilo.
 

KWA NINI ALIAMUA KUDILI NA NGOZI?
Mpashaji wetu aliliambia Amani kwamba, Wema alichoshwa na ‘vijembe’ vya watu mbalimbali wakiwemo wabaya wake kuwa ngozi yake imebabuka kwa kutumia mkorogo kupitiliza.
 
Miguu ya Wema Sepetu ‘Madam’ kabla ya kubadili ngozi.
 
“Kuna wakati Wema alikuwa akikosa amani kutokana na maneno ya watu, wengine waliokuwa wakimrushia vijembe ni masupastaa wenzake, ndiyo maana akaamua kwenda China kubadili ngozi yake iwe na mwonekano mpya,” kilisema chanzo.

Habari zaidi zilidai kwamba, supastaa huyo hakupenda kabisa Wabongo wajue kuwa yupo China kubadili ngozi, hata baadhi ya magazeti yalipoandika amekwenda kujirusha na msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ alimshukuru Mungu siri yake imesitirika.

UBADILISHAJI WA NGOZI WATUMIA SAA 12
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Wema aliingia kwenye kliniki ya ngozi katikati ya mwezi Oktoba, saa 3:12 asubuhi na shughuli ikamalizika saa 2:25 usiku.
 
“Alikaa kliniki toka saa tatu na dakika kumi na mbili asubuhi hadi saa mbili na dakika ishirini na tano usiku,” kilisema chanzo.
 
MADAKTARI WAMWONYA
Habari zaidi zinaeleza kuwa, madaktari waliokuwa wakimfanyia zoezi hilo walipomaliza walimuonya kutorudia tena kutumia mikorogo au aina yoyote ya losheni zenye kubabua ngozi, kama vile carolite.
 
SEHEMU ZILIZOHARIBIKA SANA
Kwenye mwili wa Wema, sehemu zenye mikunjo kama nyuma ya magoti, kukaribia makwapa, mapajani na mbele ya viwiko ndizo ziliongoza kwa kuharibika hali iliyokuwa ikimfanya mara nyingi ashindwe kuvaa sketi za vimini.
 

SHILINGI MILIONI 13 ZAYEYUKA
Katika zoezi hilo, Wema ambaye pia ni msanii wa filamu za Bongo na bosi wa Kampuni ya Filamu ya Endless Fame Production ya jijini Dar, ametumia shilingi za Tanzania, milioni 13 ikiwa ni pamoja na nauli yake na Bite kwenda China na kurudi, malazi na chakula.
 
APEWA DAWA YA KUZUIA KUZEEKA MAPEMA
Baada ya ubadilishaji huo wa ngozi, Wema alipewa dawa ambazo zitamsaidia kutozeeka mapema.
 
AONYWA MATUMIZI YA SIGARA NA KUTOLALA KWA WAKATI
Mbali na dawa hizo, staa huyo alionywa na matumizi ya sigara aina yoyote ile na kujipanga upya kwenye suala la kulala mapema ili apate usingizi wa kutosha.
 

MENEJA WAKE ATINGA CHINA KUHAKIKI NGOZI
Habari zaidi zikawekwa wazi kwamba, Wema alimwita meneja wake, Martin Kadinda kwa lengo la kuhakiki mwonekano mpya wa ngozi ya staa huyo.
 
Juzi, Amani lilimtafuta Dk. George wa zahanati maarufu ya Sino iliyopo Sinza Mapambano (Kwawachina) ambapo alisema warembo wengi hubadili ngozi kwa mtindo wa plastic surgery, mara nyingi sehemu yenye mikunjo au kuharibika hukatwa na kuvutwa, kama mtu alishaanza kuzeeka huonekana kijana.
 
“Nchi maarufu kwa kubadili ngozi ni Thailand, lakini China na Afrika Kusini zimeanza  kutoa huduma hiyo.
 
“Hapa nchini bingwa wa masuala ya ngozi ni Profesa Masawe, zamani alikuwa Muhimbili kwa sasa ana kituo chake upanga Dar,” alisema Dk. George.
 
Kuhusu madhara, Dk. George alisema hayako wazi sana inategemea maisha ya mtu ya kila sikiu.

MENEJA WA WEMA AZUNGUMZA
Baada ya gazeti hili kuzinyaka habari hizo, lilimtafuta meneja wa Wema, Martin Kadinda alipoulizwa alikiri kwenda China kwa ajili ya kuhakiki mwonekano mpya wa ngozi ya ‘Beautiful Onyinye’ huyo na kusema kuwa ilikuwa lazima bosi wake afanyiwe hivyo kwa sababu bosi ni kioo cha jamii.
 
“Unajua Wema ni kioo cha jamii, hivyo si vyema watu kumsema kwa kitu kidogo kuhusu ngozi yake kwani hata yeye alikuwa hapendezwi nayo. Lakini nashukuru sana kwa sasa ana mwonekano mpya wa ngozi.

“Nilikwenda kuhakikisha kama ngozi yake kwa sasa inaweza kuwa na mwonekano mpya, ni kweli wamefanikiwa madaktari. Wamempa masharti kadhaa, kama kulala sana,  lakini pia wamempa dawa nyingine,” alisema Kadinda.
 

WEMA MWENYEWE SASA
Baada ya kuzungumza na Kadinda, Amani lilimuendea hewani Wema ili kumsikia na yeye kuhusu kubadili ngozi nchini China.

Amani: Mambo Wema, za China?
Wema: Salama tu, niambie.
 
Amani: Hapa kuna habari kuwa safari yako ya China ilikuwa kwa ajili ya matengenezo ya ngozi yako, vipi ni habari za kweli?
Wema: Ah! Sasa ngozi yangu imekuaje kwani?

Amani: Inasemekana una mwonekako mpya wa ngozi, ile ya kwanza hukuipenda kwa sababu ya kujeruhiwa na mkorogo.
Wema: (kimya kidogo) oke, sikupenda kulizungumzia hilo kwa sasa lakini ndiyo hivyo kama ulivyosikia.

Amani: Unaweza kuniambia ni shilingi ngapi umetumia?
Wema: Mh! Mbona unanikaba koo jamani? Kama shilingi 
milioni 13 pamoja na gharama za usafiri.

Amani: Nashukuru sana Wema.
Wema: Karibu sana.

Chanzo: Gazeti la Amani, toleo la leo

Wastara Juma afichua siri.....Adai kioo kilimfanya amvulie nguo Sajuki



Wastara   amefichua  siri kwamba kioo ndicho kilisababisha aanzishe uhusiano wa mapenzi na marehemu Juma Issa Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki Januari 2, mwaka huu..
 
Wastara aliweka bayana kuwa marehemu Sajuki ambaye alikuwa mumewe, hakuwahi kumtongoza lakini kioo ndiyo kilikuwa chanzo kilichosababisha wajikute wameingia dhambini kwa mara ya kwanza.
 
Akizungumza na mpanda fm, Wastara alisema kuwa siku hiyo walikuwa wakifanya mazoezi ya filamu moja (hakutaja jina) nyumbani kwake na Sajuki alikuwa muongozaji wa sinema hiyo.
 
“Ilikuwa ni usiku wa manane tukiwa nyumbani kwangu tukifanya mazoezi ya filamu moja, sasa ilikuwa ni scene ya mapenzi tukawa mbele ya kioo huku tumekumbatiana.
 
“Tukaendelea hivyoo, mmh! Sasa tulivyokitazama, tukahisi tunaendana. Tukaendelea kujifanyia tathmini na ghafla tukajikuta tunafanya kweli, kioo kilisababisha tukajikuta tunafanya mapenzi,” alisema Wastara kwa uso wa aibu..

Wednesday, 23 October 2013

SERIKALI YA TANZANIA YASEMA MIKATABA YA USHIRIKIANO BAINA YA RWANDA, KENYA NA UGANDA SIO HALALI

by rahim kassonga (La Captain)

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kuwa mikataba ya ushirikiano iliyotiwa saini hivi karibuni baina ya Rwanda, Kenya na Uganda sio halali kwani makubaliano hayo yanapaswa kupitia mfumo wa sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki {EAC}.
Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka Wizara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Bi Vedastina Justinian ambaye amesisitiza kwamba mikataba iliyotiwa saini na Rwanda, Kenya na Uganda bila ya kuzishirikisha Tanzania na Burundi si halali na kwamba, ni kinyume na utaratibu wa jumuiya hiyo.
Justinian ameongeza kuwa mikataba ya Marais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda na Yoweri Museveni wa Uganda inapaswa kuidhinishwa kwanza na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na tayari serikali ya Tanzania imeuandikia rasmi uongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ikihoji kuibuka kwa utaratibu wa baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili masuala ya utangamano bila ya kuishirikisha Tanzania.
SOURCE:DAWATI
EDITOR:IRENE TEMU

SERIKALI WILAYANI MPANDA MKOANI KATAVI IMESITISHA MKATABA WA MKANDARASI

by rahim kassonga (la Captain)

Serikali Wilayani Mpanda Mkoani Katavi imesitisha mkataba wa mkandarasi katika kijiji cha Itetemya Tarafa ya Karema kwa kushindwa kujenga  jengo la shule darasa 1 na ofisi 1 aliyokuwa amepewa ndani ya miezi 2 kuanzia mwezi Septemba  hadi Novemba na kupatiwa Mkandarasi mwingine ili kuendeleza ujenzi huo.
Mkandarasi huyo amenyanganywa tenda hiyo baada ya kushindwa kukamilisha ujenzi huo licha ya kuanza msingi na kushindwa kusimamisha ukuta kutokana na kuzidiwa tenda alizonazo.
Aidha Diwani wa Kata ya Karema Maiko Kapaka amethibitisha kusitishwa kwa mkataba huo na kusema kuwa tatizo la mkandarasi huyo kushindwa kuendeleza ujenzi ni kutokuwa na mtaji wa kutosha na Mkataba ulifanyika kati ya Makao Makuu ya Hifadhi ya Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma.
SOURCE:DAWATI
EDITOR:IRENE TEMU

Tuesday, 15 October 2013

Julio amchongea Minziro Yanga

by rahim kassonga

VIJEMBE ni jambo la kawaida Ulaya hasa inapofika kwenye mechi kubwa.
Hali hiyo nayo ipo Bongo kwa Simba na Yanga wakati huu timu hizo zikijiandaa na pambano lao la Jumapili ijayo la Ligi Kuu Bara.
Sikia hii. Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekumbushia kichapo cha mabao 3-0 ambacho Yanga walikipata kutoka kwa Mtibwa Sugar msimu uliopita.
Julio alidai alipokuwa anaifundisha timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 wakiwa kambini mjini Mbeya, usiku alikutana na wachezaji wa Yanga, Mnyarwanda Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ na Athuman Idd ‘Chuji’ wakiwa baa, huku kocha wao msaidizi, Fred Minziro akishuhudia.
Julio alisema tukio hilo lilitokea baada ya Yanga kucheza na Prisons na kutoka suluhu na yeye kwa sababu alichukizwa na kitendo kile aliwasema wazi bila kuogopa.
“Kitendo kile kiliniuma, niliwaona wachezaji wale na baadhi yao ni Chuji na Niyonzima wakati walikuwa wanajua wana mechi na Mtibwa Sugar, nikiwa kama kocha wa timu ya taifa niliwasema kwa sababu iliniuma na kama nadanganya, muulizeni mwandishi huyu hapa alikuwepo (anamnyooshea kidole) akatae,” alisema Julio katika mkutano na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo, Minziro amejibu mashambulizi kwa Julio na kumwambia: “Kama yeye amemwaga mboga, mimi nitamwaga ugali kwa nini azungumze mambo ya mwaka jana ambayo si ya kweli.”
Minziro alienda mbali na kusema, sababu ya Julio kuongea mambo hayo ni hofu ya kipigo cha Jumapili na anatafuta sababu ya kuwaharibia watu majina.
“Ishu hiyo ya Mbeya, nilienda kumfuata mwanangu na ndipo nilipomkuta Julio na wachezaji na si kwamba alinikuta mimi na wachezaji,” alifafanua bila kuingia kiundani.
source:mwanaspoti

Sunday, 13 October 2013

MAAFA YAIKUMBA INDIA, MAELFU WAHAMA MAKAZI YAO


by rahim kassonga


BEHRAMPUR , India
Dhoruba kubwa imeikumba nchi ya India kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali (kimbunga) kunyesha kwenye  ukanda wa pwani ya mashariki ya India jumamosi jioni na kuleta uharibifu mkubwa wa makazi ya watu huku maelfu wakiyahama makazi yao na kutafuta hifadhi salama
wimbi kubwa likielekea pwani kwenye bandari ya Jalaripeta kwenye wilaya ya Visakhapatnam kusini mwa nchi ya India na kuharibu makazi zaidi ya 10,000

Barabara zote zilikukuwa tupu wakati mawimbi makubwa yalipoingia kwenye mwambao wa mji wa Orissa , ambao ulikumbwa na Kimbunga kikali. Jumamosi mchana. 
wanakijiji walioathiriwa na kimbunga, wakipata chakula katika hifadhi ya muda huko Chatrapur kilometa 200
Upepo mkali uliotishia hata wanaume watu wazima ulivuma kwenye mji huo. Maji ya bahari yalisukumwa kuelekea nchi kavu na kukumba vijiji vilivyokaliwa na wakulima wadogowadogo vyenye vibanda vya matope na nyasi.
wake wa wavuvi wa india wakiwaashiria waume zao (wavuvi) kurudi kufuatia dalili za kimbuka
Wakati kimbunga kikivumba kwenye mwambao wa Bengal kuelekea pwani ya Hindi, picha za  satellite zinaonyesha kimbuka hicho kinazunguka na kiini chake kufunika eneo lenye ukubwa zaidi ya Ufaransa. Picha zilionesha kuwa dhoruba kubwa ingelikumba pwani ya Gopalpur mapema jumamosi usiku
mwamvuli haukufaa kwa upepo mkali

Ikiwa na eneo kubwa lenye maji ya moto duniani, Bahari ya Hindi inachukuliwa kama chanzo cha dhoruba na baadhi ya dhoruba zilizoleta maafa makubwa kwenye siku za karibuni ilitokea kwenye pwani ya Bengal, ikiwa ni pamoja na kimbunga cha mwaka 1999 ambacho pia kiliikumba Orissa na kuua watu 10,000.
familia ikibebelea mizigo yao na kuelekea sehemu salama

Viongozi wa serikali wanasema idadi kamili ya vifo haijajulikana na itawekwa wazi siku ya jumapili.

Katika mji wa Behrampur , kilometa 10 ( maili 7 ) toka eneo la bara ambapo dhoruba ndio ilikuwa imelenga, anga liliingia giza ghafla wakati dhoruba hilo lilipotua likiwa na upepo mkali iliyoambatana na mvua nzito na kuacha mitaa yote ya mji huo ikiwa mitupu .
waathiriki wa dhoruba hiyo wakipata chakula kwenye hifadhi ya muda


Madirisha ya nyumba yalipasuka kutokana na upepo mkali. Huku vitu vya zilivyokuwa nje ya nyumba vikisikika kugonga kuta za nyumba.

"Wazazi wangu wamekuwa wakinipigia simu mara kwa mara ... walikuwa na wasiwasi sana ," alisema HEMANT PATI , 27, ambaye alikuwa kujificha katika hoteli na watu wengine 15 kutoka mji wa pwani ambao ulikuwa wa kwanza kukumbwa na dhoruba.

wanakijiji walijilinda na mvua kubwa kwa kujifunika na manailoni
Meneja wa hoteli hiyo alisema alifunga milango dhidi ya mtu yeyote kujaribu kuingia , akisema kulikuwa na chakula, maji na umeme wa jenereta tu kwa ajili ya wageni ya Jyoti Hoteli. "Hakuna mtu anaweza kuja ndani , na hakuna mtu anaweza kwenda nje," Shaik Nisaruddin alisema.

wanaume wakijarinu kuutoa mti ulioanguka barabarani kufuatia mvua na upepo mkali octoba 12
Makadirio ya nguvu ya dhoruba imeshuka kidogo,kulinganisha na taarifa ya onyo iliyotolewa na Jeshi la Maji la Marekani pamoja na kituo cha tahadhari (Typhoon Warning Centre) jijini Hawaii iliyoonyesha uwepo upepo endelevu wenye kasi ya kilomita 222 kwa saa ( 138 maili kwa saa ), na kupanda hadi 268 km/h (167  mph).

wanakijiji wa india wakipambana na upepo mkali
Ingawa dhoruba, iliendelea kuwa na nguvu nyingi mno na hatari. Saa chache kabla ya kugonga ardhi , kiini cha dhoruba hiyo kilitawanyika na kueneza upepo mkali kwenye maeneo mengi zaidi na kusababisha madhara makubwa ," alisema Jeff Masters, mkurugenzi wa hali ya hewa katika kituo binafsi cha hali ya hewa kilicho chini ya Marekani
msichana akichungulia dirishani akiwa anasafiri kwa basi kuelekea eneo salama
" Ni kitu kibaya pale kilipotua  kwenye nchi kavu, nyumba nyingi nchini India haziwezi kuhimili hata dhoruba dhaifu " Masters alisema.
Pia alisema si pwani pekee itapata uharibifu mkubwa. "Hii ni dhoruba yenye nguvu na yakushangaza, itabeba upepo wa kimbunga kuupeleka bara kwa muda wa takribani masaa 12, ambayo si kawaida kabisa  , " alisema Masters kabla ya kutokea kwa dhoruba hiyo.


Vimbunga kawaida kupoteza nguvu vinapopiga nchi kavu, ambapo kuna unyevu wenye joto dogo ambao huuathiri nishati nguvu ya dhoruba.
Ijumaa jioni, baadhi ya watu zaidi ya 420,000 walihama makazi yao kuelekea kwenye hifadhi na ardhi ya juu katika mji wa Orissa, na 100,000 zaidi katika mji jirani wa Andhra Pradesh , alisema Anil Goswami katibu wa mambo ya ndani ya Indaia.
L.S. Rathore , mkuu wa Idara ya Hali ya Hewa ya Hindi , alitabiri kuongezeka dhoruba kwa kipimo cha mita 3-3.5 ( 10-11.5 futi) , lakini watalaam kadhaa  wa Marekani walitabiri dhoruba kubwa sana ya maji na kuelekea pwani . Ryan Maue mtaalatam wa hali ya hewa toka shirika binafsi la Marekani (Weather Bell) alisema kuwa, hata katika mazingira bora, ubashiri ulionesha  kutakuwa na mawimbi ya mita 7-9 (20-30 futi).
Kuongezeka kwa dhoruba ni muuaji makubwa katika dhoruba kama ile, ingawa mvua kubwa ilichangia kuzidisha uharibifu. Serikali ya India imeisema watu milioni 12 wataathiriwa na dhoruba, ikiwa ni pamoja na mamilioni wanaoishi mbali na pwani.
Kulikuwa na taarifa chache za dhoruba huko  Orissa muda mchache baada ya dhoruba kuanza kupiga, kwa Phailin tayari kulikuwa na dhoruba kubwa kwa karibu masaa 36, na upepo mkubwa kuongezeka, alisema Maue. "Dhoruba hii kubwa haiwezi kumalizima haraka, " alisema.


Kimbunga cha mwaka 1999 kilikuwa na nguvu kama hiki cha Phailin lakini kilifunika eneo ndogo - kilirusha nje kama mita 5.9 (19.4 -futi).
Masaa kadhaa kabla ya dhoruba hii , wanakijiji wapatao 200 walikusanyika kwenye vyumba viwili, kwenye nyumba imara ya seruji shuleni katika kijiji cha Subalaya , umbali wa kilomita 30 ( maili 20 ) kutoka pwani , wakati maafisa wa mambo ya dharura ya ndani wakisambaza chakula na maji. Barabara zote zilikuwa karibu tupu, ila kwa ajili ya malori mawili kuleta misaada zaidi kwenye shule hiyo. Watoto walionekana kutetemeka na kutereza katika mvua wakiwa wanashushwa kutoka kwenye malori, wakiwafuata wanawake waliokuwa wamebeba mizigo

Wengi wenye makazi ya chini walikimbilia kwenye hifadhi , lakini baadhi yao walibaki na jamaa zao wakihofia dhoruba inaweza kuwakumba wakiwa njiani.

"Mtoto wangu alibaki na mke wake kwa sababu ya ng’ombe na mali ," alisema Kaushalya Jena mzee wa miaka 70 akilia kwa hofu ndani ya makazi ya muda. "Mimi sijui kama wao ni salama. "
Huko Bhubaneshwar na katikati ya mji wa Orissa, maafisa wa serikali na kujitolea kwa pamoja  waliweka maelfu ya mifuko ya chakula kwa ajili ya makambi ya misaada.

"Inaonekana ajabu, kwa sababu siku ilikuwa ni nzuri na jua lilikuwepo ," alisema Doris Lang wa Honolulu , ambaye alikuwa na rafiki katika mahekalu kando ya bahari kwenye mji wa Puri wakati habari za kimbunga zilipowafikia wao.
Kiongozi wa juu wa serikali, Waziri Kiongozi Naveen Patnaik , amewaasa watu kuwa watulivu .

" Naomba kila mtu  asiwe na hofu, Tafadhali isaidieni serikali . . Kila mtu kuanzia kijiji hadi makao makuu wanatakiwa kuwa na tahadhari," aliwaambia waandishi wa habari .

Surya Narayan Patro , msimamizi wa majanga , alisema kuwa "hakuna mtu ataruhusiwa kukaa katika nyumba za matope na nyasi  katika maeneo ya pwani " wakati wa dhoruba.

Hadi jumamosi mchana, bahari ilikuwa tayari imesogea nchi kavu kama umbali wa mita 40 (130 futi ) kutikea sehemu za ukanda wa pwani.






Maafisa sehemu zote mbili Orissa na Andhra Pradesh wamechukua hatua za dharura kugawa chakula, vifaa na kuanzisha vituo vya kuhifadhi watu .  Jeshi la India wameongeza nguvu juu ya hadhari hiyo,wana malori , ndege na helikopta tayari kwa ajili ya shughuli za misaada.



NEEMA YANUKIA MPANDA.....

by rahim kassonga (La Captain)
 NEEMA YANUKIA MPANDA
VIJANA WAKE MBIONI KUONEKANA LIGI KUU

Katavi imeanza kuonesha dalili za kufunguka kwenye soka baada ya wachezaji wake kuanza kuonekana nje ya mkoa huu na safari kwenye timu inazoshiriki ligi kuu

wachezaji ndugu wawili toka familia moja David Siame na mdogo wake Raphael Siame wapo mbioni kujiunga na timu kubwa hapa nchini.
kwa upande wa David Siame (kaka mtu) yupo mbioni kujiunga na klabu ya Soka ya inayoshiriki ligi kuu ya Rhino Ranger ya Tabora wakati Raphael Siame yupo mbioni kujiunga na timu ya vijana ya Simba (simba B)

wachezaji wote hao kama haitatokea tatizo lolote watajiunga na timu hizo kwenye dirisha dogo la usajili mwezi januari mwakani.
David Siame kushoto na Nassoro Maswila kulia wakiwa kwenye studio za Mpanda FM Radio

Saturday, 12 October 2013

ODOOO Aisha hussein kazini

by rahim kassonga
WATANGAZAJI WA MPANDA FM RADIO WAKIWA KAZINI
Aisha Hussein (odoo aisha) kulia akimhoji mwalimu Bernard wa Kashauriri sekondari alipokuwa akisimamia mitihani ya taifa ya kidato cha pili kwenye shule ya sekondari Mwangaza, kushoto ni Beatrice Masaki mtangazaji wa Mpanda Radio