Friday 10 January 2014

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: UCHAMBUZI WA TIMU

by rahim kassonga (La captain)
TIMU YA ARGENTINA
Argentina ni timu nzuri sana , na wanakocha bora safari hii wakiwa chini ya Alejandro Sabella na wanawachezaji bora kwenye kila idara
Mfumo wanaotumia wakumchezesha Messi chiini zaidi unaweza usiwe mzuri sana, nadhani kama wangemchezesha mbele zaidi wangefanya vema sana .
Kuna swali juu ya beki wao wa kati na golikipa Sergio Romero, lakini kwa uimara wa washambuliaji wao wanaweza kufanya vyema na hata kunyakua kombe la Dunia.

STYLE & FORMATION:
Argentina wanatumia mfumo wa 4-3-3 ingawa wakiwa ugenini hutumia  5-3-2
Mfumo wao humfanya Messi acheze kama namba 10 nyuma ya washambuliaji wawili Sergio Aguero na Gonzalo Higuain ambao hutanua sana uwanja.
Lakini wana Angel Di Maria anayetumiwa kama kama kiungo ambaye kidogo huongeza nguvu pia kwenye ulinzi.
STRENGTHS:
Wachezaji mahiri mahiri wane, Los Cuatro Fantasticos - the Fantastic Four of Di Maria, Aguero, Higuain and Messi, ambao wanauwezo wa kucheza timu yeyote duniani
Mess amekuwa akiimarika kwenye timu ya taifa, kitu kinachoonesha kwamba kama atakuwa fiti, anawezakufanya mashindano yhaya kuwa yake na kumwongezea nafasi ya kuwa mchezaji bora wa dunia wa muda wote
WEAKNESSES:
Timu haina uwiano mzuri kiufundi na haina walinzi mahiri
Goalkeeper Sergio Romero hafanyi vema na timu yake ya Monaco, huku  left-back Marcos Rojo, wa Sporting, na centre-back Federico Fernandez wa Napoli hawana uzoefu kwenye mashindano makubwa.

KEY PLAYER

Licha ya kukebehiwa kwa kutofanya vema na timu ya taifa kama anavyofanya na timu yake ya  Barcelona kwa kucheza mechi 16 za mashindano bila kufunga kocha  Alejandro Sabella alimwita Messi mwaka 2011alipoteuliwa na amekuwa ni tegemeo lake.
Messi mwenye miaka 26, amebadilika na anatoa matumaini ameshafunga magoli 20 kwenye mechi 20 alizoichezea Argentina.

MTU WA KUMWANGALIA

Angel Di Maria, kasiyake uwanjani, ufuni na nidhamuviliwafanya Real Madrid kucheza karata ya kumtoa Mesut Ozil na kumwacha yeye, wakati wakimsajili Gareth Bale.
Angel Di Maria,  25  anasifa zote za kucheza kwenye nafasi ya winga wa kushoto

THE BOSS

Alejandro Sabella alipata nafasi baada ya kuisaidia  Estudiantes  kushinda ubingwa wa Copa Libertadores.
Ni mchezaji wa zamani wa Sheffield United ya Uingereza, alikuwa sehemu ya benchi la ufundi la Argentina mwaka 98 nchini  France na ametumia muda wake mwingi wa kufundisha kama kocha msaidizi wa Daniel Passarella.

HOW THEY QUALIFIED

Argentina's qualifying campaign

  • 7 Oct 2011 W 4-1 v Chile (h)
  • 11 Oct 2011 L 0-1 v Venezuela (a)
  • 11 Nov 2011 D 1-1 v Bolivia (h)
  • 15 Nov 2011 W 2-1 v Colombia (a)
  • 2 Jun 2012 W 4-0 v Ecuador (h)
  • 7 Sep 2012 W 3-1 v Paraguay (h)
  • 11 Sep 2012 D 1-1 v Peru (a)
  • 12 Oct 2012 W 3-0 v Uruguay (h)
  • 16 Oct 2012 W 2-1 v Chile (a)
  • 22 Mar 2013 W 3-0 v Venezuela (h)
  • 26 Mar 2013 D 1-1 v Bolivia (a)
  • 7 Jun 2013 D 0-0 v Colombia (h)
  • 11 Jun 2013 D 1-1 v Ecuador (a)
  • 10 Sep 2013 W 5-2 v Paraguay (a)
  • 11 Oct 2013 W 3-1 v Peru (h)
  • 15 Oct 2013 L 2-3 v Uruguay (a)
Wamedungwa kwa mara ya kwanza na  Venezuela, na kutoa sare nyumbani na Bolivia wakati walifungwa mchezo wa mwisho ambao haukuwa na umuhimu sana kwao dhidi ya Uruguay kwani walikuwa wamekwishafuzu.

WORLD CUP RECORD

Mabingwa mwaka 1978 na 1986, washindi wapili mwaka 1930 na 1990, wameshindwa kufika nusu fainali katika mashindano matano ya mwisho.

Fifa ranking: 3                                                                  

No comments:

Post a Comment