Wednesday 22 January 2014

Shule ya msingi  Mpanda  inakabiliwa na changamoto mbalimbali  ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa  na matundu ya vyoo ukilinganisha na idadi ya watoto  wanaosoma katika shule hiyo.
Hayo yamebainishwa na mwalimu mkuu wa shule Bw. Lazaro Jangu wakati akizungumza na mwandishi wa habari  ofisini kwake amesema kuwa,baadhi ya watoto hulazimika  kukaa chini wakati wamasomo hali ambayo inawawia vigumu walimu kufundisha.
Vilevile amesema kuwa licha ya madarasa ya kufundishia kuwa machache  wanafunzi wa awali  na darasa la kwanza  mpaka sasa wamefikia jumla ya mia tatu arobaini na mbili ambapo wanabanana na mwalimu kukosa sehemu ya kusimama wakati akufundisha.
Aidha Bw.Jangu ameomba wazazi  kuweza kuwahimiza wanafunzi ambao mpaka sasa hawajafika shuleni ili kujiunga na wenzao  kwani walio wengi wamekuwa wakiwatumia watoto wao kwenye shughuli zingine za nyumbani.

SOURCE:TRYPHONE

No comments:

Post a Comment