Tuesday 1 July 2014

Mke wa T.I amkimbia Floyd Mayweather kwenye BET Red Carpet


Mke wa rapper T.I, Tiny hakutaka ugomvi mwingine utokee kwenye tuzo za BET baada ya kumkimbia kiaina bondia Mayweather aliyekuwa anajaribu kumuita.
Video iliyochukuliwa na na Hip Hollywood inamuoenesha Floyd Mayweather akijaribu kumuita Tiny wakati wapo wote kwenye red carpet, lakini Tiny anaonesha kushitukia na kukatisha interview yake haraka kisha akaondoka.
Bado Mayweather alionesha nia ya kutaka kumgusa mkono lakini Tiny aliendelea kuchapa mwendo na kujiunga na T.I.
Hata hivyo baada ya kuingia ukumbini, mchekeshaji Chris Rock ambaye alikuwa MC  aliendelea kufanya utani kuhusu ugomvi wa T.I na Mayweather uliotokea mwezi mmoja uliopita baada ya Mayweather kuonekana akiwa na Tiny kwenye picha kadhaa kitendo ambacho hakikumfurahisha kabisa rapper huyo.

No comments:

Post a Comment