Saturday 30 November 2013

PICHA ZA MPANDA FM

TID ALALA MAHABUSU

by zangii ze icon


 
Khaleed Mohamed 'TID'.
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Khaleed Mohamed 'TID' yupo mahabusu katika Kituo cha Polisi Oysterbay tangu jana usiku baada ya kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi msichana anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake,  Mariam Nnauye.

BAADA YA KUFUKUZWA KWA KUFANYA NGONO NDANI YA GARI YA WEMA SEPETU..PRODUZA HUYO AMENENA MAZITO NA MADUDU YA WEMA SEPETU NA KAMPUNI YAKE


BY ZANNGII ZE ICON

Baada ya juzi kati kuripotiwa habari ya aliyekuwa producer ama mtengenezaji wa vipindi vya Wema Sepetu Chidi Mohamed kufukuzwa kazi kutokana na kulitumia gari la kampuni kama sehemu yake ya kuvunjia amri ya sita na wadada wa mjini, hatimaye katika pitapita zetu za mtandaoni tuliweza kukutana na kauli ya producer huyo akizungumzia habari hiyo ya yeye kufukuzwa kazi kwenye kampuni ya Endless Fame ya wema sepetu.

Chidi mwenyewe anasema kuwa habari hizo si za kwel na ni kwamba wote walioandika wamepanga kumchafua tuu kwa kuogopa kuwa anaweza kuyaniika mambo mazito yanayoendelea huko endless Fame
Kwa mujibu wa chidi anasema kuwa yeye ameondoka kwenye Kampuni hiyo siyo kwa sababu ya uzinzi ngani ya gari kama ilivyoripotiwa bali ni kutokana na sababu hizi kuu mbili.
1. Ameona hamna jipya na wala hamna maendeleo yoyote ndani ya Kampuni hiyo ndio maana ameamua kuondoka

2. Wafanyakazi wa Endless Fame hawalipwi kabisa ndio maana yeye akaamua kujitoa kwani anafanya kazi bure na pia sio yeye peke yake aliyeondoka bali kuna wafanyakazi zaidi ya watatu walioondoka kwenye kampuni hiyo ila nashangaa ni kwanini wameamua kumchafua yeye?
Bado tunafanya mawasiliano na Endless Fame ili tujue kama daia haya ni ya kweli au la......


Thursday 28 November 2013

UKWELI WA ISHU YA SNURA NA MRISHO NGASSA.

BY ZANGII ZE ICON

Ni picha ambazo zimekua zikizungumziwa kwenye mitandao ya kijamii na hata kwenye mitandao
mingine ya habari nchini Tanzania zikimwonyesha mchezaji wa Yanga Mrisho Ngassa akiwa mapenzini na mwimbaji Snura wa bongofleva.

Snura anasema mwanzo wa hizi picha kusambaa ni baada ya kupoteza simu yake, namnukuu akisema ‘hizo picha hazina uhusiano wowote unaounganishwa kimapenzi kati yangu na Ngassa ila ni sehemu ya vipande vya movie yangu inaitwa ‘Majanga’ ambayo nimeanza kuifanya na Ngassa amecheza ndani yake kwenye scene za mapenzi, yani Snura kwenye movie amecheza kama binti mrembo anaerukiarukia Wanaume’

‘Simu yangu ilipotea ndio maana wamezipata hizo picha, wakati tunashoot tulikua tunapigapiga tu hayo mapicha, mi sikuwa nataka kuzitoa kabisa manake movie yenyewe bado naifanya nusunusu kutokana na kukosa muda, hii ishu imeniletea sana matatizo manake mwingine anakua haamini unachokiongea na hakuna kitu kinauma kama kuongea ukweli alafu mtu anasema unadanganya’ – Snura

Kwa kumalizia Snura anasema ‘Ngassa alinipiga muda mfupi tu baada ya picha kuanza kusambaa akauliza mbona hizi picha zinasambaa hivi Snura? nikamwambia usinielewe tofauti babaangu kwa sababu mimi mwenyewe sikutaka zitoke, picha nilizopiga nyinginyingi tu wakati tunatengeneza movie ila naona watu wameona hizi ndio nzuri kwa skendo’ 

WAZEE KATAVI WASHAURI SERIKALI KUENDELEA NA OPERESHENI TOKOMEZA UJANGILI




MWAMLIMA-DC

Wazee Mkoani Katavi wameshauri Serikali kuendelea na operation tokomeza ujangili kwa kuwa imesadia kwa kiasi kikubwa kuokoa rasilimali za Taifa zilizokuwa zikiteketea kutokana na baadhi ya watu wachache waliokuwa wakijihusisha na ujangili wa kuhujumu rasilimali hizo.
Wakiongea kwenye Mkutano Maalum wa majadiliano na Wazee wakiwa na  Mkuu wa Wilaya Mpanda Paza Mwamlima  wamezungumzia  juu ya wahamiaji haramu nao wanajihususha kwa njia moja au nyingine na   katika vitendo vya ujangili na uharibifu wa mazingira wamesema hali hiyo ikiendelea uharibifu wa rasilimali za Taifa kama wanyama pori na mistu,  na  uharibifu wa mazingira hali inayoashiria    kutoweka  kwa  rasilimali  za taifa.

Kwa upande wake Mkuu huyo wa Wilaya  ya Mpanda Paza Mwamlima amesema katika   operation tokomeza  ujangili iliyofanyika Mkoani  Katavi  katika Wilaya ya Mpanda  Kata  moja  ya Mwese pekee jumla ya silaha 250 zilikamatwa hiyo inaonesha ni namna gani watu wanaishi na silaha ambazo hutumika kwa vitendo vya ujangili hivyo amewaomba wazee hao kusaidia kwa njia moja au nyingine kuwafichua watu wa namna hiyo wanaojihusisha na  uharifu, akaongeza  kuwa wazee ni tunu ya Taifa na amani katika nchi Wazee wanasaidia katika kuimarisha amani.
Awali katika risala yao wazee walimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa usafiri wa kuwafikia wenzao walioko mbali kutoka makao makuu ya wilaya na Mkoa kuwafikia wazee wenzao walioko wilaya ya Mlele na Kata za Inyonga, mamba. Majimoto, kasansa kibaoni ,usevya mwamapuli,mbede,ikuba, Nsenkwa, Ilelea, Ilunde na Utende
Pia alitaja wazee wengine walioko katika kata za mwese, karema ,ikola,  Mishamo katuma Kapalamsenga na sibwesa pamoja  na maeneo mengine imekuwa tatizo kuwafikia hivyo wanaomba kusaidiwa kutatua changamotohiyo.
Changamoto nyingine waliyozungumzia  ni wazee kutohudumiwa ipasavyo hususani wanpokuwa wakipatiwa matibabu katika Hospitali wakaeleza kuwa wanakumbana na vikwazo vingi,pia wakaomba kusamehewa na mambo mengine kama kulipia umeme na huduma nyingine.
Mmoja wa wazee aliyejitambulisha kwa jina la John Kisalala aliomba eneo la kusaidia wazee matibabu liwekewe utaratibu mzuri ili kuondoa usumbufu kwa wazee hao ikiwa ni pamoja na kuondolewa usumbufu wa kulipia huduma ya maji, umeme na huduma nyingine kwa kuwa wazee hao wamelitumika taifa kwa muda mrefu na sana na sasa wanatakiwa kuhudumiwa.
Akizungumzia operation tokomeza ujangilia na operation kimbunga wazee hao wameshauri washirikishwe katika zoezi hilo kwa kuwa wazee wanawatambua watu ambao sio wazawa wao wanawatambua watu ambao siyo raia halali.
Naye Benezite Mwanauta akizungumzia uharibifu wa mazingira na rasilimali za taifa amewalaumu wafungaji wa kabilia la kisukuma kwa kukataa miti hovyo huku watu waliopewa dhamana wakiwa wanaangali bila kuchukua hatua yeyote  huku mazingira yakiendelea kuharibika suala hilo lisipochukuliwa hatua na umuhimu wa kipeke huenda katavi ikageuka jangwa walishauri hatua za makusudi zichukuliwe ili kunusuru uharibifu huo.
sikiliza hapa
http://www.hulkshare.com/356bxvkxsp1c

HUYU NDIO MSANII WA VITUKO SHOW ALIYEPIGWA NA MKE WAKE KIPIGO CHA PAKA MWIZI.

by zangii ze icon

HUYU ndiye msanii  niliyemzungumzia wiki iliyopita kuhusu kichapo alichopewa kama mnavyomuona hapo pichani.


Anatambulika kwa
jina  ''Kazi Kijeba''.. MSANII kutoka kundi la BONGO SUPERSTAR'S COMEDY linalorusha kipindi chake maarufu hapa nchini (VITUKO SHOW) Kinachorushwa katika runinga ya CHANNEL TEN Kundu  hili limeweka kambi ya takribani miaka miwili mkoani Tanga.

Nafikiri chazo cha habari cha wiki iliyopita hakikufafanua kisa kwa kina,tuliweza kuongea na msanii huyu na kugundua kwamba aliyemdunda kumbe alikuwa mpenzi wake anaeishi maeneo ya usagara Jijini Tanga, Na sio mara moja alishawahi kumpiga tena mara ya kwanza wakaachana baadae kama mnavyojua mapenzi, Si wakarudiana tena?.. Ila hii ya sasahivi hakuwa na nia njema maana alimpigia kelele za mwizi hatimaye msanii huyu kunusurika kufa aliokolewa na muuza bucha baada ya kukimbilia buchani..! Ama kweli wanawake wa sikuhizi noma...! Yani weka jiwe niweke kigingi.

HAYA NDIO MAJANGA YALIYOMKUTA TUNDA MAN HUKO TABORA HIVI KARIBUNI.


by zangii ze icon


Msanii wa kizazi kipya - Tunda Man pichani alijikuta akishangiliwa sana na kupata wakati mgumu wa kujipenyeza popote aliposhuka kwenye
gari siku ya tarehe 23.11.2013 kwenye tamasha la uzinduzi wa somo la TEHAMA mkoani Tabora katika uwanja wa Al-hassan Mwinyi, jeshi la polisi lilitakiwa kutoa msaada kwa msanii huyo kwani wanafunzi wengi wa shule za msingi waliohudhuria tamasha hilo walimzonga hali iliyotatanisha ikiwa watadondoka na kuanza kukanyagana.

[chini utaitazama video hiyo-KWA KIASI WALIHARIBU HATA UTARATIBU WA UCHUKUAJI WA VIDEO HIYO KWA SHAUKU YA KUMWONA MSANII WAO]


Akitathimini fadhira za wanafunzi kumshangilia...





wakati akiondoka na kuwaaga




Wanafunzi hawakuridhika na walizidi kulizonga gari wakati akiondoa na ilikuwa vigumu kuwazuia.

Thursday 21 November 2013

UNESCO YAITAKA SERIKALI KUZITAMBUA REDIO ZA JAMII NCHINI

DSC05297
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (kushoto) akiwasili katika Hoteli ya New Palm Tree iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani kufungua mkutano wa nne wa Mtandao wa vyombo vya habari vya Kijamii nchini (COMNETA) akiwa ameongozana na wenyeji wake Afisa Mipango Taifa wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari na mratibu wa miradi ya UNESCO , Yusuph Al-Amin (wa pili kulia), Mwenyekiti wa COMNETA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO Bw.Joseph Sekiku (wa pili kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa COMNETA ambaye pia ni Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Telecentre Sengerema FM mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye.
Na.Mwandishi wetu
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni,(UNESCO), limeiomba Serikali kutambua mchango wa redio za jamii katika maendeleo nchini na hivyo kufanya nao kazi kwa karibu.
Ombi hilo limetolewa jana na Afisa Mipango Taifa wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari na mratibu wa miradi ya UNESCO , Yusuph Al-Amin wakati wa mkutano wa Mtandao wa vyombo vya habari vya Kijamii nchini (Community Media Network of Tanzania – COMNETA)unaofanyika mjini Bagamoyo.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Al-Amin aliwapongeza COMNETA kwa kufanikiwa kuanzisha umoja huo ambao awali kulikuwa na vituo viwili tu vilivyokuwa vikitambuliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), huku kwa sasa vikifikia vituo zaidi ya 27, kwa nchi nzima ikiwemo Tanzania Bara na Visiwani.
DSC05299
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akibadilishana mawazo na wenyeji wake kabla ya kufungua mkutano wa nne wa COMNETA unaoendelea Bagamoyo mkoa wa Pwani.
Akifafanua zaidi, Al-Amin alisema UNESCO imekuwa ukiisaidia COMNETA kufikia malengo yake kwa kutambua kuwa radio hizo zinafanya kazi katika jamii na zina uwezo mkubwa wa kuifikia jamii inayoizunguka.
“Zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania wako vijijini na hawa wanafikiwa kwa karibu zaidi na radio jamii, kwa kupata taarifa za kina na za haraka” alisema Al-Amin.
Alitoa mfano wa Radio ya jamii iliyoko Micheweni, Pemba ambayo uwepo wake umesaidia sana kuleta mabadiliko ya maendeleo wilayani hapo tofauti na ilivyokuwa huko nyuma ambapo wilaya hiyo likuwa nyuma sana kimaendeleo.
‘Vipindi mbalimbali vya kuhamasisha maendeleo vinavyorushwa na redio hii vimesaidia sana kuhamasisha wananchi na sasa mwamko wa maendeleo umekuwa mkubwa hapo Micheweni” alisema, Al-Amin.
DSC05318
Mwenyekiti wa COMNETA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO Bw.Joseph Sekiku akizungumza na WanaCOMNETA kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene.
Aliwashauri wanachama wa COMNETA, wawe na umoja, mshikamano na kupendana ili kuepuka migogoro inayoweza kuyumbisha ustawi wa chama. “Tunawaomba sana, COMNETA, muwe mfano wa kuigwa kwa kuepuka migongano ya wenyewe kwa wenyewe ikiwamo kugombea madaraka ili kuwa umoja wa mfano kwa katika tasnia ya vyombo vya habari hapa nchini’.
Kwa upande wake, mgeni rasmi katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene aliupongeza umoja huo na kuwataka kuendelea kuwa daraja muhimu la kuipasha jamii mambo yote ya msingi bila kuvunja misingi ya kitaifa ikiwemo kulinda maslahi ya taifa.
“Kwanza kabisa, niwapongeze, COMNETA kwa kuanzisha umoja wenu huu, na kuwapo kwangu hapa leo kunanifunza mengi, hivyo kwa yale yote mulioniomba nami, nitayafikisha kwa wahusika na kuyafanyia kazi” alisema, Mwambene.
Aidha, akijibu maswali mbali mbali ya wajumbe yaliyokuwa yakitolewa kwenye mkutano huo, Mwambene aliwahakikishia kuwa Serikali inatambua mchango wa vyombo vya habari na inatarajia kupeleka muswada wa sheria ya vyombo vya habari kwenye Bunge lijalo.
“Muswada wa habari upo tayari, tunatarajia utapelekwa Bungeni katika kikao kijacho mwezi Desemba ili kujadiliwa.Tunaamini Kamati husika ya Bunge itawakaribisha wadau wa tasnia ya habari ili kutoa mawazo yao katika muswada huo kabla haujafikishwa bungeni,” alisema.
DSC05335
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akitoa risala wakati akifungua mkutano wa siku nne wa COMNETA unaoendelea mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani.
DSC05357

Akidokeza juu ya yaliyomo ndani ya muswada huo, Mwambene alisema umebainisha wazi ulazima wa wamiliki wa vyombo vya habari kuwakatia bima za afya na usalama kazini waajiriwa wao pamoja na suala la maslahi stahiki kwa waandishi wa habari. Muswada huo pia umependekeza kiwango cha elimu kwa mwandishi wa habari kiwe shahada ya kwanza.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa COMNETA, Bw. Felician Nchewe aliomba Serikali ivifikirie vyombo vya Jamii nchini, katika kufikia malengo yake.
DSC05408
Afisa Mipango Taifa wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari na mratibu wa miradi ya UNESCO, Bw.Yusuph Al-Amin akizungumza mbele ya mgeni rasmi Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nne wa WanaCOMNETA uliofunguliwa rasmi jana wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.
“Kwa sasa COMNETA, tumefikia malengo mbali mbali, hivyo tunaiomba sana Serikali ivifikie vyombo hivi vya Jamii, kama ilivyo kwa wenzetu kupitia TCRA, kuvisaidia vituo vya Tele Centre kufikia malengo yao” alisema Nchewe.
Kwa upande wake, Mkufunzi wa radio za Jamii kutoka UNESCO, Mama Rose Hajj Mwalimu alisema mkutano huo wa COMNETA wa siku nne, ni wa kuweka mifumo na mikakati bora ya uendashaji wa vituo hivyo na kuweka maazimio ya kufanyia kazi. Ambapo uliwahusisha Mameneja na Wakurugenzi kutoka radio za Jamii (Community Radio) zilizopo nchini.
Mkutano huo unaendelea katika hoteli ya New Palm Tree Village, Bagamoyo.
DSC05371
Meneja wa Redio Kahama FM Marco Mipawa akichangia maoni yake juu ya sheria ya Magereza wakati wa mkutano wa nne wa COMNETA unaohusisha redio za Jamii nchini uliofadhiliwa na Shirika la UNESCO kupitia mradi wa DEP.
DSC05384
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akitoa maoni yake katika mkutano huo
DSC05303
Baadhi ya washiriki wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa mkutano wa nne wa COMNETA unaoendelea Bagamoyo mkoani Pwani.
DSC05272
Erick Kalunga kutoka Ubalozi wa Uswiss ambao wanadhamini mradi wa SIDA akizungumzia furaha yao kuona miradi wanayofadhili inapiga hatua na kuleta maendeleo kwa jamii.
DSC05432
Mwenyekiti wa Tanzania Telecentre Network (TTN) Bw. Hirnoy Barmeda akizungumzia umuhimu wa Telecentre kwa jamii.
DSC05441
Mkurugenzi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Barmedas na Jamii Foundation Crystal Kigoni akifafanua kuhusu taasisi yao isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na mambo ya ustawi wa Jamiikupitia vyombo vya habari na Teknohama kwa kuibua mambo yanayotokea mitaani kwa jamii inayozunguka Redio za Jamii.
DSC05446
Washiriki wa mkutano wa nne wa COMNETA unaoendelea wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
DSC05453
Mkutano wa nne wa WanaCOMNETA ukiendelea katika hoteli ya New Palm Tree wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.
DSC05450
Mratibu wa Mtandao wa Jinsia na Habari Tawi la Tanzania (GEMSAT) Bi. Gladness Hemedi Munuo akiongelea usawa wa jinsia katika Uongozi na Utawala kwa Redio za Jamii.
IMG_4988
Mshauri wa UNESCO, Balozi mstaafu Mh. Celestine Liundi akisisitiza umuhimu wa kuhubiri amani kwa redio za Jamii nchini.
DSC05265
Meneja wa mradi wa DEP kutoka UNESCO Courtney Ivins akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa COMNETA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO Bw.Joseph Sekiku kwenye mkutano wa WanaCOMNETA unaoendelea wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.
DSC05422
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene katika picha ya pamoja na WanaCOMNETA mara baada ya kufungua mkutano wa nne wa COMNETA wilayani Bagamoyo.
DSC05425
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene katika picha ya pamoja na Bodi ya COMNETA.
DSC05420
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (kulia) akibadilishana mawazo na Mshauri wa UNESCO, Balozi mstaafu Celestine Liundi (katikati) pamoja Mkufunzi wa Mafunzo hayo ambaye pia ni Mjumbe ya wadhamini COMNETA Bw. Gervas Mushiro (kushoto)

Monday 18 November 2013

THE VOICE OF KATAVI: KATAVI SPORTS BONANZA

THE VOICE OF KATAVI: KATAVI SPORTS BONANZA: by rahim kassonga
Tamasha kubwa la aina  yake na la kwanza la michezo limefanyika leo wilayani Mpanda mkoani Katavi kwa kushir...

KATAVI SPORTS BONANZA


by rahim kassonga
Tamasha kubwa la aina  yake na la kwanza la michezo limefanyika leo wilayani Mpanda mkoani Katavi kwa kushirikisha michezo  mbalimbali ikiwemo,mpira wa miguu kwa wanawake,wanaume na watoto,mpira wa pete,mpira wa wavu,riadha ,kukimbia na magunia,kufukuza kuku,mbio za walemavu na kushindana kunywa soda.
Tamasha  hilo lililofanyika katika viwanja vya azimio lilianza saa tatu asubuhi na kumalizika saa kumi na mbili jioni ambapo kamanda wa polisi mkoa wa katavi,Dhahiri Kidavashari ndiye alikuwa mgeni rasmi ambapo alitia baraka katika tamasha hilo kwa kupiga penati na kumfunga muhandisi Frank John wa Tanroad.
Katika hotuba yake kamanda Kidavashari alisisitiza kuwa michezo ni afya,michezo ni ajira lakini pia michezo inaleta undugu kwani inawakusanya watu pamoja na  kuongeza kuwa kama michezo ikitumika vizuri inapunguza uhalifu.
kikosi cha msakila
kikosi cha shule ya Uhuru
timu ya Msakila na Uhuru wakikaguliwa na waamuzi





Afisa michezo halmashauri ya mji-Revocatus Kalunde akifungua Bonanza
waamuzi wa mchezo wa ufunguzi, Daudi (kushoto), Ngalla (katikati) na Kaburu (kulia) wakiingia uwanjani tayari kwa mchezo wa ufunguzi
vijana wa msakila wakisalimiana kabla ya mchezo
kibatari nishati, the super MC akisherehesha



mchezaji wa Msakila akimiliki mpira
vijana wa Msakila wakimpongeza mwenzao baada ya kufunga goli
wanafunzi wa Msakila wakishangilia baada ya mpira kwisha na kuibuka washindi
Ulinzi ulikuwa wa kutosha


timu ya netiboli ya halmashauri ya wilaya ikifanya mazoezi kabla ya kuanza kwa mchezo huo

pasha..pasha..pasha

Timu ya vijana ikipokea maelekezo toka kwa mwalimu wao
MAELEKEZO
Timu za netiboli zikipokea maelekezo kabla ya kuanza kwa mchezo

KIVUMBI KIMEANZA
huwezi amini hadi mapumziko walikuwa wamefungana 16-16





Mkubwa ni mkubwa, mwishowe Halmashauri ya wilaya waliibuka na ushindi

SARAKASI
mambo ya sarakasi pia yalikuwepo, ilikuwa noumaaa sanaaaaaaaaaaaaaaa


WATU WENGIIIIIIIIIIIII
watoto kwa wakubwa, wanawake kwa wanaume


KUFUKUZA KUKU
mtu aliondoka na bonge la jogoo, ilikuwa nouma sanaa, weka mbali na watoto

wanaume wakijiandaa kufukuza kuku

refarii akitoa maelekezo

kuku anapasha
KAZI IMEANZA HATARIIIIIIIIIIIIIIIIIIII

HATIMAE JAMAA KAJIPATIA KITOWEO, kiroho safi




BURUDANI KADHAA ZILITO;EWA, mshikamano arts group nao waliwasha moto




RIADHA MITA 400 KINAMAMA  ilikuwa sooo,





HATARII SANAAA, jamaa akionesha mautundu kwa kucheza na baiskeli huwezi amini, mshikaji alivyotembelea tairi moja


KWENYE VOLLEYBALL NAKO PALIKUWA HAPATOSHI
veta na katavi walioneshana kazi




WEKA MBALI NA WATOTO, mbio za magunia zilifunika

kazi imeanza
huyu jamaa nouma sana, achana nae

soka la wanawake
AMSHA POPO, watoto wakipiga viduku