Thursday 28 August 2014

HAYA NDIO MAKUBWA USIYOYAJUA KUHUSU MZIWANDA NA SHILOLE NI HATARI TUPU

STAA wa Bongo Fleva, Nuh Naftari Mlawa ‘Nuh’ amefunguka ya moyoni kuhusiana na kipaji chake na kusema kuwa ‘sexy lady’ wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ndiye aliyempa mwanga kunako gemu ya Bongo Fleva.Akikisanua kupitia Global TV Online juzikati, Mziwanda alimshukuru Shilole na kuongeza pia kujichora kwake mchoro mkononi wenye jina la bidada huyo ni kuweka historia kuwa alishawahi kutokea mtu wa muhimu maishani mwake.

“Zamani nilikuwa nafanya muziki lakini nyota yangu haikung’aa kihivyo, baada ya kumpata Shilole nyota zetu zikaonekana kuwa sawa hivyo nikang’aa japo mapenzi ndiyo yaliyotuunganisha,” alisema Mziwanda.

No comments:

Post a Comment