Friday 29 August 2014

MUME WA MTU: SIMUACHI NG’O AUNT


Mcheza shoo wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond,’ Moses Iyobo amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kuenea uvumi wa kutoka kimapenzi na mcheza filamu mahiri Bongo, Aunt Ezekiel kuwa hawezi kumuacha msanii huyo ng’o.
Mcheza shoo wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond,’ Moses Iyobo (katikati).
Akizungumza  hivi karibuni, Moses alisema kuwa kutokana na maneno mengi kuenea kuwa anatoka na Aunt, ameona ni bora aweke wazi hisia zake kwamba ni kweli anampenda msanii huyo na kuwa naye mbali itakuwa vigumu.
Mcheza filamu mahiri Bongo, Aunt Ezekiel.
“Mengi yameongelewa sana sasa naweka wazi kuwa nampenda sana Aunt. Unajua kama mtu haukuwa na uhusiano naye mara unaanza kusikia vitu vya ajabu bora tu ufanye kweli hata kama wanakusema wakuseme kihalali na si vitu ambavyo si vya kweli,” alisema dansa huyo ambaye ni mume wa mwanamke aliyefahamika kwa jina moja la Mwegi.

No comments:

Post a Comment