Thursday, 24 October 2013

Wastara Juma afichua siri.....Adai kioo kilimfanya amvulie nguo Sajuki



Wastara   amefichua  siri kwamba kioo ndicho kilisababisha aanzishe uhusiano wa mapenzi na marehemu Juma Issa Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki Januari 2, mwaka huu..
 
Wastara aliweka bayana kuwa marehemu Sajuki ambaye alikuwa mumewe, hakuwahi kumtongoza lakini kioo ndiyo kilikuwa chanzo kilichosababisha wajikute wameingia dhambini kwa mara ya kwanza.
 
Akizungumza na mpanda fm, Wastara alisema kuwa siku hiyo walikuwa wakifanya mazoezi ya filamu moja (hakutaja jina) nyumbani kwake na Sajuki alikuwa muongozaji wa sinema hiyo.
 
“Ilikuwa ni usiku wa manane tukiwa nyumbani kwangu tukifanya mazoezi ya filamu moja, sasa ilikuwa ni scene ya mapenzi tukawa mbele ya kioo huku tumekumbatiana.
 
“Tukaendelea hivyoo, mmh! Sasa tulivyokitazama, tukahisi tunaendana. Tukaendelea kujifanyia tathmini na ghafla tukajikuta tunafanya kweli, kioo kilisababisha tukajikuta tunafanya mapenzi,” alisema Wastara kwa uso wa aibu..

Wednesday, 23 October 2013

SERIKALI YA TANZANIA YASEMA MIKATABA YA USHIRIKIANO BAINA YA RWANDA, KENYA NA UGANDA SIO HALALI

by rahim kassonga (La Captain)

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kuwa mikataba ya ushirikiano iliyotiwa saini hivi karibuni baina ya Rwanda, Kenya na Uganda sio halali kwani makubaliano hayo yanapaswa kupitia mfumo wa sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki {EAC}.
Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka Wizara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Bi Vedastina Justinian ambaye amesisitiza kwamba mikataba iliyotiwa saini na Rwanda, Kenya na Uganda bila ya kuzishirikisha Tanzania na Burundi si halali na kwamba, ni kinyume na utaratibu wa jumuiya hiyo.
Justinian ameongeza kuwa mikataba ya Marais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda na Yoweri Museveni wa Uganda inapaswa kuidhinishwa kwanza na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na tayari serikali ya Tanzania imeuandikia rasmi uongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ikihoji kuibuka kwa utaratibu wa baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili masuala ya utangamano bila ya kuishirikisha Tanzania.
SOURCE:DAWATI
EDITOR:IRENE TEMU

SERIKALI WILAYANI MPANDA MKOANI KATAVI IMESITISHA MKATABA WA MKANDARASI

by rahim kassonga (la Captain)

Serikali Wilayani Mpanda Mkoani Katavi imesitisha mkataba wa mkandarasi katika kijiji cha Itetemya Tarafa ya Karema kwa kushindwa kujenga  jengo la shule darasa 1 na ofisi 1 aliyokuwa amepewa ndani ya miezi 2 kuanzia mwezi Septemba  hadi Novemba na kupatiwa Mkandarasi mwingine ili kuendeleza ujenzi huo.
Mkandarasi huyo amenyanganywa tenda hiyo baada ya kushindwa kukamilisha ujenzi huo licha ya kuanza msingi na kushindwa kusimamisha ukuta kutokana na kuzidiwa tenda alizonazo.
Aidha Diwani wa Kata ya Karema Maiko Kapaka amethibitisha kusitishwa kwa mkataba huo na kusema kuwa tatizo la mkandarasi huyo kushindwa kuendeleza ujenzi ni kutokuwa na mtaji wa kutosha na Mkataba ulifanyika kati ya Makao Makuu ya Hifadhi ya Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma.
SOURCE:DAWATI
EDITOR:IRENE TEMU

Tuesday, 15 October 2013

Julio amchongea Minziro Yanga

by rahim kassonga

VIJEMBE ni jambo la kawaida Ulaya hasa inapofika kwenye mechi kubwa.
Hali hiyo nayo ipo Bongo kwa Simba na Yanga wakati huu timu hizo zikijiandaa na pambano lao la Jumapili ijayo la Ligi Kuu Bara.
Sikia hii. Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekumbushia kichapo cha mabao 3-0 ambacho Yanga walikipata kutoka kwa Mtibwa Sugar msimu uliopita.
Julio alidai alipokuwa anaifundisha timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 wakiwa kambini mjini Mbeya, usiku alikutana na wachezaji wa Yanga, Mnyarwanda Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ na Athuman Idd ‘Chuji’ wakiwa baa, huku kocha wao msaidizi, Fred Minziro akishuhudia.
Julio alisema tukio hilo lilitokea baada ya Yanga kucheza na Prisons na kutoka suluhu na yeye kwa sababu alichukizwa na kitendo kile aliwasema wazi bila kuogopa.
“Kitendo kile kiliniuma, niliwaona wachezaji wale na baadhi yao ni Chuji na Niyonzima wakati walikuwa wanajua wana mechi na Mtibwa Sugar, nikiwa kama kocha wa timu ya taifa niliwasema kwa sababu iliniuma na kama nadanganya, muulizeni mwandishi huyu hapa alikuwepo (anamnyooshea kidole) akatae,” alisema Julio katika mkutano na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo, Minziro amejibu mashambulizi kwa Julio na kumwambia: “Kama yeye amemwaga mboga, mimi nitamwaga ugali kwa nini azungumze mambo ya mwaka jana ambayo si ya kweli.”
Minziro alienda mbali na kusema, sababu ya Julio kuongea mambo hayo ni hofu ya kipigo cha Jumapili na anatafuta sababu ya kuwaharibia watu majina.
“Ishu hiyo ya Mbeya, nilienda kumfuata mwanangu na ndipo nilipomkuta Julio na wachezaji na si kwamba alinikuta mimi na wachezaji,” alifafanua bila kuingia kiundani.
source:mwanaspoti

Sunday, 13 October 2013

MAAFA YAIKUMBA INDIA, MAELFU WAHAMA MAKAZI YAO


by rahim kassonga


BEHRAMPUR , India
Dhoruba kubwa imeikumba nchi ya India kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali (kimbunga) kunyesha kwenye  ukanda wa pwani ya mashariki ya India jumamosi jioni na kuleta uharibifu mkubwa wa makazi ya watu huku maelfu wakiyahama makazi yao na kutafuta hifadhi salama
wimbi kubwa likielekea pwani kwenye bandari ya Jalaripeta kwenye wilaya ya Visakhapatnam kusini mwa nchi ya India na kuharibu makazi zaidi ya 10,000

Barabara zote zilikukuwa tupu wakati mawimbi makubwa yalipoingia kwenye mwambao wa mji wa Orissa , ambao ulikumbwa na Kimbunga kikali. Jumamosi mchana. 
wanakijiji walioathiriwa na kimbunga, wakipata chakula katika hifadhi ya muda huko Chatrapur kilometa 200
Upepo mkali uliotishia hata wanaume watu wazima ulivuma kwenye mji huo. Maji ya bahari yalisukumwa kuelekea nchi kavu na kukumba vijiji vilivyokaliwa na wakulima wadogowadogo vyenye vibanda vya matope na nyasi.
wake wa wavuvi wa india wakiwaashiria waume zao (wavuvi) kurudi kufuatia dalili za kimbuka
Wakati kimbunga kikivumba kwenye mwambao wa Bengal kuelekea pwani ya Hindi, picha za  satellite zinaonyesha kimbuka hicho kinazunguka na kiini chake kufunika eneo lenye ukubwa zaidi ya Ufaransa. Picha zilionesha kuwa dhoruba kubwa ingelikumba pwani ya Gopalpur mapema jumamosi usiku
mwamvuli haukufaa kwa upepo mkali

Ikiwa na eneo kubwa lenye maji ya moto duniani, Bahari ya Hindi inachukuliwa kama chanzo cha dhoruba na baadhi ya dhoruba zilizoleta maafa makubwa kwenye siku za karibuni ilitokea kwenye pwani ya Bengal, ikiwa ni pamoja na kimbunga cha mwaka 1999 ambacho pia kiliikumba Orissa na kuua watu 10,000.
familia ikibebelea mizigo yao na kuelekea sehemu salama

Viongozi wa serikali wanasema idadi kamili ya vifo haijajulikana na itawekwa wazi siku ya jumapili.

Katika mji wa Behrampur , kilometa 10 ( maili 7 ) toka eneo la bara ambapo dhoruba ndio ilikuwa imelenga, anga liliingia giza ghafla wakati dhoruba hilo lilipotua likiwa na upepo mkali iliyoambatana na mvua nzito na kuacha mitaa yote ya mji huo ikiwa mitupu .
waathiriki wa dhoruba hiyo wakipata chakula kwenye hifadhi ya muda


Madirisha ya nyumba yalipasuka kutokana na upepo mkali. Huku vitu vya zilivyokuwa nje ya nyumba vikisikika kugonga kuta za nyumba.

"Wazazi wangu wamekuwa wakinipigia simu mara kwa mara ... walikuwa na wasiwasi sana ," alisema HEMANT PATI , 27, ambaye alikuwa kujificha katika hoteli na watu wengine 15 kutoka mji wa pwani ambao ulikuwa wa kwanza kukumbwa na dhoruba.

wanakijiji walijilinda na mvua kubwa kwa kujifunika na manailoni
Meneja wa hoteli hiyo alisema alifunga milango dhidi ya mtu yeyote kujaribu kuingia , akisema kulikuwa na chakula, maji na umeme wa jenereta tu kwa ajili ya wageni ya Jyoti Hoteli. "Hakuna mtu anaweza kuja ndani , na hakuna mtu anaweza kwenda nje," Shaik Nisaruddin alisema.

wanaume wakijarinu kuutoa mti ulioanguka barabarani kufuatia mvua na upepo mkali octoba 12
Makadirio ya nguvu ya dhoruba imeshuka kidogo,kulinganisha na taarifa ya onyo iliyotolewa na Jeshi la Maji la Marekani pamoja na kituo cha tahadhari (Typhoon Warning Centre) jijini Hawaii iliyoonyesha uwepo upepo endelevu wenye kasi ya kilomita 222 kwa saa ( 138 maili kwa saa ), na kupanda hadi 268 km/h (167  mph).

wanakijiji wa india wakipambana na upepo mkali
Ingawa dhoruba, iliendelea kuwa na nguvu nyingi mno na hatari. Saa chache kabla ya kugonga ardhi , kiini cha dhoruba hiyo kilitawanyika na kueneza upepo mkali kwenye maeneo mengi zaidi na kusababisha madhara makubwa ," alisema Jeff Masters, mkurugenzi wa hali ya hewa katika kituo binafsi cha hali ya hewa kilicho chini ya Marekani
msichana akichungulia dirishani akiwa anasafiri kwa basi kuelekea eneo salama
" Ni kitu kibaya pale kilipotua  kwenye nchi kavu, nyumba nyingi nchini India haziwezi kuhimili hata dhoruba dhaifu " Masters alisema.
Pia alisema si pwani pekee itapata uharibifu mkubwa. "Hii ni dhoruba yenye nguvu na yakushangaza, itabeba upepo wa kimbunga kuupeleka bara kwa muda wa takribani masaa 12, ambayo si kawaida kabisa  , " alisema Masters kabla ya kutokea kwa dhoruba hiyo.


Vimbunga kawaida kupoteza nguvu vinapopiga nchi kavu, ambapo kuna unyevu wenye joto dogo ambao huuathiri nishati nguvu ya dhoruba.
Ijumaa jioni, baadhi ya watu zaidi ya 420,000 walihama makazi yao kuelekea kwenye hifadhi na ardhi ya juu katika mji wa Orissa, na 100,000 zaidi katika mji jirani wa Andhra Pradesh , alisema Anil Goswami katibu wa mambo ya ndani ya Indaia.
L.S. Rathore , mkuu wa Idara ya Hali ya Hewa ya Hindi , alitabiri kuongezeka dhoruba kwa kipimo cha mita 3-3.5 ( 10-11.5 futi) , lakini watalaam kadhaa  wa Marekani walitabiri dhoruba kubwa sana ya maji na kuelekea pwani . Ryan Maue mtaalatam wa hali ya hewa toka shirika binafsi la Marekani (Weather Bell) alisema kuwa, hata katika mazingira bora, ubashiri ulionesha  kutakuwa na mawimbi ya mita 7-9 (20-30 futi).
Kuongezeka kwa dhoruba ni muuaji makubwa katika dhoruba kama ile, ingawa mvua kubwa ilichangia kuzidisha uharibifu. Serikali ya India imeisema watu milioni 12 wataathiriwa na dhoruba, ikiwa ni pamoja na mamilioni wanaoishi mbali na pwani.
Kulikuwa na taarifa chache za dhoruba huko  Orissa muda mchache baada ya dhoruba kuanza kupiga, kwa Phailin tayari kulikuwa na dhoruba kubwa kwa karibu masaa 36, na upepo mkubwa kuongezeka, alisema Maue. "Dhoruba hii kubwa haiwezi kumalizima haraka, " alisema.


Kimbunga cha mwaka 1999 kilikuwa na nguvu kama hiki cha Phailin lakini kilifunika eneo ndogo - kilirusha nje kama mita 5.9 (19.4 -futi).
Masaa kadhaa kabla ya dhoruba hii , wanakijiji wapatao 200 walikusanyika kwenye vyumba viwili, kwenye nyumba imara ya seruji shuleni katika kijiji cha Subalaya , umbali wa kilomita 30 ( maili 20 ) kutoka pwani , wakati maafisa wa mambo ya dharura ya ndani wakisambaza chakula na maji. Barabara zote zilikuwa karibu tupu, ila kwa ajili ya malori mawili kuleta misaada zaidi kwenye shule hiyo. Watoto walionekana kutetemeka na kutereza katika mvua wakiwa wanashushwa kutoka kwenye malori, wakiwafuata wanawake waliokuwa wamebeba mizigo

Wengi wenye makazi ya chini walikimbilia kwenye hifadhi , lakini baadhi yao walibaki na jamaa zao wakihofia dhoruba inaweza kuwakumba wakiwa njiani.

"Mtoto wangu alibaki na mke wake kwa sababu ya ng’ombe na mali ," alisema Kaushalya Jena mzee wa miaka 70 akilia kwa hofu ndani ya makazi ya muda. "Mimi sijui kama wao ni salama. "
Huko Bhubaneshwar na katikati ya mji wa Orissa, maafisa wa serikali na kujitolea kwa pamoja  waliweka maelfu ya mifuko ya chakula kwa ajili ya makambi ya misaada.

"Inaonekana ajabu, kwa sababu siku ilikuwa ni nzuri na jua lilikuwepo ," alisema Doris Lang wa Honolulu , ambaye alikuwa na rafiki katika mahekalu kando ya bahari kwenye mji wa Puri wakati habari za kimbunga zilipowafikia wao.
Kiongozi wa juu wa serikali, Waziri Kiongozi Naveen Patnaik , amewaasa watu kuwa watulivu .

" Naomba kila mtu  asiwe na hofu, Tafadhali isaidieni serikali . . Kila mtu kuanzia kijiji hadi makao makuu wanatakiwa kuwa na tahadhari," aliwaambia waandishi wa habari .

Surya Narayan Patro , msimamizi wa majanga , alisema kuwa "hakuna mtu ataruhusiwa kukaa katika nyumba za matope na nyasi  katika maeneo ya pwani " wakati wa dhoruba.

Hadi jumamosi mchana, bahari ilikuwa tayari imesogea nchi kavu kama umbali wa mita 40 (130 futi ) kutikea sehemu za ukanda wa pwani.






Maafisa sehemu zote mbili Orissa na Andhra Pradesh wamechukua hatua za dharura kugawa chakula, vifaa na kuanzisha vituo vya kuhifadhi watu .  Jeshi la India wameongeza nguvu juu ya hadhari hiyo,wana malori , ndege na helikopta tayari kwa ajili ya shughuli za misaada.



NEEMA YANUKIA MPANDA.....

by rahim kassonga (La Captain)
 NEEMA YANUKIA MPANDA
VIJANA WAKE MBIONI KUONEKANA LIGI KUU

Katavi imeanza kuonesha dalili za kufunguka kwenye soka baada ya wachezaji wake kuanza kuonekana nje ya mkoa huu na safari kwenye timu inazoshiriki ligi kuu

wachezaji ndugu wawili toka familia moja David Siame na mdogo wake Raphael Siame wapo mbioni kujiunga na timu kubwa hapa nchini.
kwa upande wa David Siame (kaka mtu) yupo mbioni kujiunga na klabu ya Soka ya inayoshiriki ligi kuu ya Rhino Ranger ya Tabora wakati Raphael Siame yupo mbioni kujiunga na timu ya vijana ya Simba (simba B)

wachezaji wote hao kama haitatokea tatizo lolote watajiunga na timu hizo kwenye dirisha dogo la usajili mwezi januari mwakani.
David Siame kushoto na Nassoro Maswila kulia wakiwa kwenye studio za Mpanda FM Radio

Saturday, 12 October 2013

ODOOO Aisha hussein kazini

by rahim kassonga
WATANGAZAJI WA MPANDA FM RADIO WAKIWA KAZINI
Aisha Hussein (odoo aisha) kulia akimhoji mwalimu Bernard wa Kashauriri sekondari alipokuwa akisimamia mitihani ya taifa ya kidato cha pili kwenye shule ya sekondari Mwangaza, kushoto ni Beatrice Masaki mtangazaji wa Mpanda Radio

Friday, 11 October 2013

MPANDA FM RADIO NDANI YA MAHAFALI KATUMBA

Na: rahim kassonga (La Captain)

UONGOZI WA MPANDA FM RADIO, WAALIKWA KAMA WAGENI RASMI KWENYE MAHAFALI HUKO TAMBAZI (makazi ya wakimbizi katumba)

msafara wa Mpanda FM radio ukiwa kwenye ofisi za mkuu wa makazi katumba, kwa ajii ya kujitambulisha na kupata kibali cha kuingia makazi

Tunu Lugombe akifanya yake wakati Mpanda FM radio wakisubiri hatua za  ofisi ya makazi




Babuu the suka akipoza mtambo wake baada ya kuvunja rekodi ya kutembea dakika 18 Mpanda -Katumba

Msafara wa Mpanda FM radio upo Tambazi-Katumba kwenye shule ya msingi Tambazi 
Mgeni rasmi, meneja wa Mpanda FM radio akiingia eneo la tukio

waalikwa Mpanda FM radio wakiwa meza kuu, tayari kwa kuanza ratiba za mahafali yaliyofana sana

meza kuu wapili kulia ni mkuu wa shule, katikati mgeni rasmi

baadhi ya wanafunzi wa Tambazi na waagwa

wanafuzi wa Tambazi wakifuatilia kwa makini utaratibu mzima

baadhi ya wahitimu

wanaTambazi na baadhi ya wanafunzi waliohudhuria mahafali hiyo

mchungaji akifungua mahafali kwa maombi

wananchi wa Tambazi wakisikiliza kwa makini maneno toka meza kuu

mkuu wa shule akitambulisha watumishi wake kwa mgeni rasmi

mtangazji wa Mpanda radio akituma tukio hilo live radioni, huku akipata ulinzi mkali toka kwa bodyguard (kassonga)

Captain kassonga akiwa kazini

meneja wa mpanda FM radio na Tunu Lugombe wakiwa meza kuu

waagwa wa shule ya msingi Tambazi 2013, wakitoa burudani

mapanga shaaaaaaaa, pia yalikuwepo

waagwa akiyakata mapanga

burudani za kutosha zilikuwepo

pozi za graduuuuuuu

ngonjera nazo hazikuwa nyuma

wanafunzi darasa la kwanza hadi la tatu akiburudisha kwa ngonjera

watangazaji wa Mpanda FM radio wakifuatilia burudani kwa makini

meneja wa Mpanda FM radio akiwa makini na matukio ya graduuuuu

pozi la menejaaaaaaaaaaaaaaaa

MC wa tukio hilo alikuwa na makeke mengi na kutoa burudani ya aina yake hapa akiwa kwenye poziiii

wanafunzi waagwa akitoa burudani

sio kama wamechoka bali ni pozi la umakini wa matukio

burudani zilipochanganya, meza kuu ilishindwa kujizuia kwa kucheka

wahitimu wakisoma risala kwa mgeni rasmi

mgeni rasmi akijiandaa kupokea risala

mgeni rasmi akipokea risala toka kwa waagwa

baada ya kusoma risala, waagwa aliondoka kwa kustua kijoti na kutoa burudani babu kubwa

mgeni rasmi akiipitia risala na kunong'ona kitu na tunu lugombe

mgeni rasmi anatoa zawadi ya mwanafunzi bora kwa upande wa taaluma

mtoto wa mwalimu lazima awe na akili, hapa mtoto wa mwalimu na mama yake akipokea zawadi 

bodyguard yupo makini na kazi yake

mwanafunzi aliyepokea zawadi ya usafi akipongezwa na walimu wake na kupewa zawadi ya  vyoda

zawadi zikiendelea kutolewa

meza kuu ilipomaliza kutoa zawadi

kutoa zawadi kazi hadi kiu!!!!!!!!!

waagwa akisikiliza nasaha kwa makini na nidhamu ya hali ya juu

waagwa akishangilia nasaha nzuri toka kwa mgeni rasmi Meneja wa Mpanda FM radio

mwanafunzi huyu alikuwa burudani na kuwavutia wengi kwani
alikuwa mcheshi, akihusika kila tukio, bingwa wa viduku lakini pia aliwafunika wanafunzi wenzake wote
kitaaluma .....kweli wanawake wanaweza

meneja wa Mpanda FM radio Gerard Seti Sedekia akitoa hutuba kwenye mahafali

menejaaaaa, tabasam hilooooooooooo

mkuu wa shule na meneja Seti wakiwa tayari kwa picha ya pamoja na kupokea zawadi toka  waagwa

hapa katika picha ya pamoja

    meneja baada ya kupokea zawadi toka kwa waagwa


serikali mpo wapi?????   oneni shule yenu hii imeisahau? darasa hili ni baadhi ya madarasa machache yanayohitaji ukarabati shuleni Tambazi

usafiri wetu

wazazi wakibebelea zawadi tayari kuwapa waagwa

mtangazaji wa mpanda fm radio akiwa kwenye tanki la maji ambalo linatumika kuvunia maji ya mvua na huu ni mfano wa kuigwa kwa shule zingine

ni kama utaliii


pozi la bodyguardddddddddddd