Sunday 22 September 2013

Formula 1 – Perez hahofii kuhusu mustakabali wa baadae na kampuni ya McLaren



Dereva Sergio Perez amesisitiza kuwa hahofii mustakabali wake wa baadae na kampuni McLaren, japokuwa team hiyo imeweka bayana mpango wao wa kumleta dereva Fernando Alonso kwa ajili ya kumbadilisha nae


Mkuu wa team ya McLaren Martin Whitmarsh ameweka bayana nchini Singapore kwenye Singapore Grand Prix kwamba team inataka kuona mabadiliko chanya toka Perez kabla ya kumpa mkataba mwingine mwakani.
Na kuongeza kuwa mtu ambaye anatakiwa kwa kuchukua nafasi yake ni dereva mmexixo Alonzo ambaye alishasema kwamba asingependa kurudi kwenye timu hyo hivi karibuni
Perez alisema hajahusishwa kuhusu suala hilo na anauhakika atakuwepo kwenye timu ya Mc Laren mwakani
Aliongeza kuwa, unatakiwa kufanya kazi kwa bidii kwenye timu yoyote utakayokuwepo, siku zote unatakiwa kufanya vema zaidi na kitaalam
Akizungumzia kuhusu kauli ya bosi wake amesema kuwa, kauli hiyo ya Whitmarsh ni kauli ya kumwamsha ili aongeze juhudi
"ndio kitu ninachofanya na najaribu kutoa kitu nilichonacho kwa ufanisi wa hali ya juu, umekuwa wakati mgumu msimu huu kwetu sote, lakini kila siku nasema maisha yangu ya baadae hapa yapo sawa
Nitakuwepo hapa mwaka ujao na ngoja tuone, ninaimani tutarudi na kupigania ubingwa mwaka ujao

No comments:

Post a Comment