Tuesday 15 April 2014

SHETA ASIMULIA ALIVYOPATA AJALI



MWISHONI mwa wiki  iliripotiwa juu ya msanii Shetta kupata ajali mbaya ya gari wakati akielekea Babati, mkoani Manyara kwa ajili ya kazi za muziki ingawa aliweza kunusurika katika ajali hiyo.
Akizungumza na Pro-24 msanii huyo alielezea kisa kizima kilichopelekea kutokea kwa ajali hiyo mkoani huko ambapo ilisababisha kazi hiyo ya muziki kushindwa kufanyika mkoani hapo.
Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ilikuwa ni kumkwepa Pundamilia aliyekuwa akikatiza barabarani hali iliyopelekea kpata ajali mbaya ingawa anamshukuru mungu kuwa hivi sasa yupo salama.
"Nilitumia usafiri wa ndege kutoka Dar es Salaam, hadi Arusha ambapo nilikuwa na kazi huko Babati kufika sehemu inayoitwa Minjingo ambapo sehemu hiyo inakuwa na wanyama wengi kidogo , tulikutana na Pundamilia mmoja barabarani alikuwa ameshavuka sasa wakati gari pia haijavuka nae alikuwa anataka kurudi tena huko halafu gari lilikuwa kwenye mwendo kasi kidogo" alisema Sheta.
Sheta ameeleza kuwa gari limeumia sana lakini wao wamenusurika ingawa bado anamaumivu ya kawaida ambapo hivi sasa yupo hospitali kwa ajili ya kupima afya yake kama anamaumivu yoyote ndani .
Ameweka wazi kuwa kutokana na ajali hiyo imebidi show yake iahirishwe kwa kuwa kila mtu alikuwa amepata taarifa kuhusu ajali hiyo hivyo hakuwa na sababu yoyote ya kuendelea na show hiyo zaidi ya kuimarisha afya yake kwanza.

No comments:

Post a Comment