Wazee
Mkoani Katavi wameshauri Serikali kuendelea na operation tokomeza
ujangili kwa kuwa imesadia kwa kiasi kikubwa kuokoa rasilimali za Taifa
zilizokuwa zikiteketea kutokana na baadhi ya watu wachache waliokuwa
wakijihusisha na ujangili wa kuhujumu rasilimali hizo.
Wakiongea
kwenye Mkutano Maalum wa majadiliano na Wazee wakiwa na Mkuu wa Wilaya
Mpanda Paza Mwamlima wamezungumzia juu ya wahamiaji haramu nao
wanajihususha kwa njia moja au nyingine na katika vitendo vya ujangili
na uharibifu wa mazingira wamesema hali hiyo ikiendelea uharibifu wa
rasilimali za Taifa kama wanyama pori na mistu, na uharibifu wa
mazingira hali inayoashiria kutoweka kwa rasilimali za taifa.
Kwa
upande wake Mkuu huyo wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima amesema katika
operation tokomeza ujangili iliyofanyika Mkoani Katavi katika
Wilaya ya Mpanda Kata moja ya Mwese pekee jumla ya silaha 250
zilikamatwa hiyo inaonesha ni namna gani watu wanaishi na silaha ambazo
hutumika kwa vitendo vya ujangili hivyo amewaomba wazee hao kusaidia kwa
njia moja au nyingine kuwafichua watu wa namna hiyo wanaojihusisha na
uharifu, akaongeza kuwa wazee ni tunu ya Taifa na amani katika nchi
Wazee wanasaidia katika kuimarisha amani.
Awali
katika risala yao wazee walimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa wanakabiliwa na
changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa usafiri wa kuwafikia wenzao
walioko mbali kutoka makao makuu ya wilaya na Mkoa kuwafikia wazee
wenzao walioko wilaya ya Mlele na Kata za Inyonga, mamba. Majimoto,
kasansa kibaoni ,usevya mwamapuli,mbede,ikuba, Nsenkwa, Ilelea, Ilunde
na Utende
Pia
alitaja wazee wengine walioko katika kata za mwese, karema ,ikola,
Mishamo katuma Kapalamsenga na sibwesa pamoja na maeneo mengine imekuwa
tatizo kuwafikia hivyo wanaomba kusaidiwa kutatua changamotohiyo.
Changamoto
nyingine waliyozungumzia ni wazee kutohudumiwa ipasavyo hususani
wanpokuwa wakipatiwa matibabu katika Hospitali wakaeleza kuwa
wanakumbana na vikwazo vingi,pia wakaomba kusamehewa na mambo mengine
kama kulipia umeme na huduma nyingine.
Mmoja
wa wazee aliyejitambulisha kwa jina la John Kisalala aliomba eneo la
kusaidia wazee matibabu liwekewe utaratibu mzuri ili kuondoa usumbufu
kwa wazee hao ikiwa ni pamoja na kuondolewa usumbufu wa kulipia huduma
ya maji, umeme na huduma nyingine kwa kuwa wazee hao wamelitumika taifa
kwa muda mrefu na sana na sasa wanatakiwa kuhudumiwa.
Akizungumzia
operation tokomeza ujangilia na operation kimbunga wazee hao wameshauri
washirikishwe katika zoezi hilo kwa kuwa wazee wanawatambua watu ambao
sio wazawa wao wanawatambua watu ambao siyo raia halali.
Naye
Benezite Mwanauta akizungumzia uharibifu wa mazingira na rasilimali za
taifa amewalaumu wafungaji wa kabilia la kisukuma kwa kukataa miti hovyo
huku watu waliopewa dhamana wakiwa wanaangali bila kuchukua hatua
yeyote huku mazingira yakiendelea kuharibika suala hilo lisipochukuliwa
hatua na umuhimu wa kipeke huenda katavi ikageuka jangwa walishauri
hatua za makusudi zichukuliwe ili kunusuru uharibifu huo.
sikiliza hapa
http://www.hulkshare.com/356bxvkxsp1c
No comments:
Post a Comment