Monday 28 October 2013

JINI KABULA AAMUA "KUOKOKA"...ASHINDA NA BIBLIA

MWANADADA anayefanya vizuri kunako gemu la filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ameamua kubadili mfumo wa maisha kwa kusoma Biblia kila wakati.
 
Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’.
Paparazi wetu alimnasa Jini Kabula nyumbani kwake Sinza akiwa anasoma Biblia na alipoulizwa kulikoni amekuwa mtu wa kushinda nyumbani na siyo kupiga misele kama alivyozoeleka, alitiririka:
“Nimeamua kubadili mfumo wa maisha yangu niliyokuwa nikiishi zamani ya kuendekeza starehe, nimemrudia Mungu wangu na mara nyingi nashinda ndani kwangu nikisoma Biblia kwa sababu Mungu ndiye rafiki wa kweli,” alisema Jini Kabula.

No comments:

Post a Comment