Saturday 26 October 2013

Ofisi ,usafiri,nyumba za wafanyakazi vyazorotesha huduma za elimu

by rahim kassonga (La Captain)


KATAVI
Chama cha walimu (CWT) Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi  kimetoa changamoto wanazo kabiliana nazo na malengo ambayo wanatarajia kufanya ili kuimarisha chama hicho.

Akiongea na Mpanda Fm Mwenyekiti wa chama hicho Mwl. Kenedi Simsokwe amesema kuwa mazingira ya uendeshaji ni magumu kwakutokuwa na Ofisi ya chama,usafiri,nyumba za wafanyakazi na baadhi ya wanachama kuto kufikisha marejesho shuleni.

Aidha Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa  malengo ambayo wanayo ni kuongeza huduma zaidi kwa wanachama kwa kuwatembelea mara kwa mara na kujenga ofisi ya chama ili kuweza kufanya kazi kwa ufasaha.

Hata hivyo Simsokwe amesema kuwa anaiomba serikali iwatambue na kuwathamini walimu kwa kuwaongezea posho kama inavyo fanya kwa watumishi wengine wa umma sambamba na kuboresha mazingira ya kazi kwa kufanya hivyo watakuwa wameinua kiwango cha elimu Mkoani hapa . 
SOURCE:DAWATI
EDITOR:IRENE TEMU

No comments:

Post a Comment