Tuesday 21 October 2014

Breaking News kuhusiana na hukumu ya Pistorius? miaka 5 jela Isome hapa



Pistorius III 
Kesi iliyokuwa ikimkabili mwanariadha wa nchini Afrika Kusini, Oscar Pistorius hatimaye imefikia ukingoni ambapo Mahakama ya jijini Pretoria imemkuta na hatia ya mauaji ya bila kukusudia.
Kutokana na kukutwa na hatia hiyo, mahakama ikiongozwa na jaji Thokozile Masipa imeamuru Pistorius atumikie kifungo cha miaka 5 jela.
Wakati wa kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo, ndugu wa Pistorius walionesha kukata tamaa japo waliahidi kusimama pamoja na Pistorius bila ya kujali hukumu gani itaamriwa na mahakama hiyo.
Mwanariadha huyo amekutwa na hatia hiyo baada ya kushitakiwa kwa kesi ya kumuua kwa kumpiga risasi aliyekuwa mchumba Wake, Reeva Steenkamp tarehe 14 Februari, 2013.

No comments:

Post a Comment