Wednesday 1 October 2014

WAZEE WALALAMIKIA KUNYANYAPALIWA NA WAHUDUMA WA AFYA

Wazee wakiwa kwenye kongamano la wazee kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mpanda kujadili changamoto zinazowakabili wakati wa kupatiwa matibabu.
.
Wahudumu wa Afya wameendelea kuwanyanyapaa wazee wawapo hospitalini kupata huduma ya Afya kwa kuwaacha wakae asubuhi hadi jioni ,huku wenyewe wakifanya kazi zao nyingine.
Pia wakitibiwa na Daktari mara nyingi huambiwa wakatafute dawa madukani hata kama zipo hospitalini na ukiuliza kwa nini hujibu hawahitaji usumbufu.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Shirika la Wazee saidia lenye makao yake Wilayani Kasulu Mkoani Cotlida Kokupima wakati akiwasilisha salamu za wazee kutoka Mkoani kigoma kwenye kongamano la wazee lililofanyika Mjini Mpanda Mkoa wa Katavi.
Bibi Kokupima ameeleza changamoto zinazowakabiliwa wazee katika maeneo mbalimbali zikiwemo na manyanyaso hayo wanayofanyiwa wazee wakiwa katika Zahanati,Vituo vya Afya Pamoja na Kwenye Hospitali mbalimbali hapa nchini.
Changamoto hizo ni kuwa wakienda kutibiwa na wakishaandikiwa dawa wanaambiwa hazipo waende wakanunue madukani wakati mwingine wanakuwa hawana hela matokeo yake wanarudi nyumbani kulala bila kupata dawa na mwisho ni kufa.
Changamoto ya usafiri kutoka nyumba hadi kufika kwenye huduma za jamii hasa matibabu kwa wazee wenye umri mkubwa ni taabu,hawana uwezo wa kuzifuata dawa dukani hata kama watakuwa na fedha.
Kwa Upande wake mwakilishi wa shirika la Afya la Wazee Duniani Athman Daniel ameeleza kuwa shirika lake kwa kusaidiana na wadau mbalimbali na wazee limeweza kuchangia kuisukuma serikali kuona uwezekano wa kuwapatia wazee malipo ya uzeeni na mchakato unaenda vizuri na wakati wowote suala hilo litafanikiwa.
Akizungumzia Halmashauri ya Mpanda amesifu juhudi zilizofanywa katika kuwahudumia wazee kwa kutenga chumba cha kiliniki ya wazee na wanapatiwa huduma hapo.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “WAZEE WASIACHWE NYUMA TUJENGE JAMII SHIRIKISHI KUPITISHA SHERIA YAO.

No comments:

Post a Comment