Hali ya taharuki
iliibuka katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kwale nchini Kenya,
baada ya mwanamume mmoja kwenda ukumbini na kuanza kutandika bakora
kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza
densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la
Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Walikuwa wameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy,
Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Mwanamume huyo alimshambulia Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani
na kumchapa mara mbili kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na pia
kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na
walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanammume huyo alimshambulia Raila ila baadhi
wabnasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza
densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika
kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu.
No comments:
Post a Comment