Jumatano Septemba 25
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Birmingham v Swansea
Manchester United v
Liverpool
Newcastle v Leeds
Tranmere v Stoke
[Saa 4 Usiku]
West Brom v Arsenal
Nicklas Bendtner
anatarajiwa kuichezea Arsenal kwa mara ya kwanza baada ya Miaka miwili wakati
Arsenal watakaposafiri kwenda kucheza na West Brom kwenye Mechi ya Raundi ya
Tatu ya Capital One Cup.
Tangu ajiunge na
Arsenal Mwaka 2005, Bendtner ameshindwa kutulia na kupata Namba ya kudumu na
mara 3 ametolewa nje kwa Mkopo.
Kabla Msimu huu
kuanza, Bendtner alilazimika kurudi tena Arsenal baada ya kushindwa kupata
Klabu ya kuhamia.
Uwezekano wa Bendtner
kucheza Mechi na West Brom ulitolewa na Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ambae
alisema: “Jumatano tuna Mechi na West Brom A ya Capital One Cup na Bendtner ana
nafasi kucheza. Kubadilisha Kikosi ni muhimu kwani Jumamosi tunacheza na kisha
inakuja Mechi muhimu mno na Napoli ya UFA CHAMPIONZ LIGI.”
Mara ya mwisho
Bendtner kuichezea Arsenal ni Agosti 2011 walipofungwa 2-0 na Liverpool na
baada ya hapo alipelekwa kwa Mkopo huko Sunderland na Juventus.
Lakini mara baada ya
kuchukuliwa kwa mkopo wa Msimu mzima na Sunderland hapo Mwaka 2011, Bendtner
alitamka: “Sitarudi tena Arsenal. Ikiwa ni juu yangu, sitacheza nao tena!”
Wakati huohuo
Inaaminika kuwa Robin van Persie hatakuwepo kwenye mchezo wa leo dhidi ya liverpool baada ya kuumia kabla ya mchezo na man city jumapili
No comments:
Post a Comment