Monday 30 September 2013

LIONEL MESSI: AUMIA WAKATI BARCELONA IKIENDELEZA REKODI YA KUSHINDA MECHI SABA MFULULIZO

by rahim kassonga



Messi Lionel alitolewa baada ya kuumia mguu wakati Barcelona ikiwapiga Almeria 2-0 huku akiweka rekodi ya klabu hiyo kushinda michezo saba mfululizo ya ligi mwanzoni mwa msimu

 Muargentina huyo , ambaye alifunga goli lake la nane kwenye ligi msimu huu anatarajiwa kufanyiwa vipimo jumanne wiki hii

Mbrazil Adriano ndiye aliyeipatia Barca bao la pili 'baada ya mapumziko baada ya kuunganisha krosi hafifu ya Fabrigas

Messi, 26, ambaye alionekana mbele ya hakimu wa Kihispania ijumaa katika kesi inayomkabilia ya udanganyifu wa kodi aliiwezesha Barcelona kuongoza katika dakika ya 21, alipopiga shuti kali umbali wa yadi 20, lakini dakika nane baadae alitolewa baada ya kuumia

Gerardo Martino, ambaye aliteuliwa kuwa kocha wa Barca katika majira ya joto, amezishinda rekodi zilizowekwa na mameneja wengine watano waliomtangulia akiwemo  - Pep Guardiola (2009-10) na Tito Vilanova (2012-13) ambao walifanikiwa kuanza kwa kushinda michezo 6 mfululizo



Baada ya mchezo mbazili ADRIANO alisema kuhusu majereuhi ya Messi kuwa ninaimani sio makubwa na atakuwa nasi katika michezo ijayo. Aliongeza kuwa Messi ni mchezaji bora na muhimu, timu inakamilika na kuwa tofauti mkiwa nae
Lakini taarifa toka ndani ya klabu hiyo zinasema mchezaji huyo atakaa nje kwa wiki 2 hadi 3

No comments:

Post a Comment