Wednesday 25 September 2013

MAONI YA SHABIKI WA MAN UNITED: MOYES ASIRUDIE MAKOSA AU TUJIANDAE NA AIBU YA KUKOSA CHAMPIONS LEAGUE MSIMU UJAO

by rahim kassonga


Nilinyanyuka kwenye kochi la nyumbani kwangu nikiwa mzito na kwenda kulala moja kwa moja ikiwa ni mapema sana kuliko kawaida yangu. Hii ilikuwa baada ya kuangalia timu yangu niipendayo ikadhalilishwa katika dimba la Etihad usiku wa jumapili ya wiki iliyopita. Nilijiuliza swali moja tu hivi ni kweli hata kuna ushindani mkubwa msimu huu kama inavyosemekana baina ya vilabu viwili vya jiji la Manchester.

Vilabu vyote viwili vinajinasibu kwamba vipo katika muda wa mapito baada ya kubadilisha makocha, lakini ushindi wa 4-1 wa City dhidi ya majirani zao ulionyesha utofauti mkubwa uliopo baina ya vikosi vya klabu hizi mbili.

City wana ukamilifu kwenye idara, ubora wa ufundi, na matamanio ya dhati ya kurudisha ubingwa wa Premier League chini ya kocha mwenye ufundi mkubwa hasa kwenye mechi kubwa kama hizi. 
MSIMAMO WA PREMIER LEAGUE 
TIMU

1. Arsenal
2. Tottenham
3. Man City
4. Chelsea
......................
5. Liverpool
6. Everton
7. Southampton
8. Man Utd

MECHI

5
5
5
5
........
5
5
5
5

GD

5
4
8
4
........
2
2
1
1
Points

12
12
10
10
........
10
9
8
7
Katika michezo mitano ya ligi ambayo tayari Man United tumeshacheza, inaonekana wazi inabidi tubadilike sana au tusihau kuhusu ubingwa na kuweka kipaumbele katika kumaliza ndani ya TOP 4.

David Moyes alipewa ratiba ngumu - na hata akalalamika kuhusu ratiba hiyo ngumu - lakini mscotish huyu amepata pointi moja tu katika michezo yote mitatu tuliyocheza na timu kubwa zenye upinzani nasi katika ligi na kikosi chake kimecheza kwa kiwango cha kuridhisha kwenye mchezo mmoja tu wa ligi.

Ukiachana na mchezo wa kufungua ligi dhidi ya Swansea, United tumekuwa tukionekana kukosa ubora wa pamoja kama timu, huku safu yetu ya ulinzi ikiyumba hasa kwa viwango vya wachezaji wetu wenye umri mkubwa kiasi kama Rio Ferdinand na Patrice Evra.

Ujio wa Marouane Fellaini katika siku ya mwisho ya usajili ulikuwa muhimu sana, lakini United bado wana tatizo sana katika safu ya kiungo - hawana uimara wa kuweza kufananisha na safu ya kiungo cha Chelsea, City, Tottenham, na sasa hata Arsenal wanaoringia ujio wa 'The Master of Assists' Mesut Ozil na mkabaji Matheiu Flamini.

Kitu kingine cha kuhuzunisha ni upangaji wa kikosi wa kocha, inaonekana bado anafanya majaribio wakati wapinzani wetu wengine wanaogombea TOP 4 wakiwa wameanza vizuri ligi, pamoja na kwamba wamebadilisha makocha na wengine hata wakiwa wameuza wachezaji mategemeo katika msimu uliopita.

United sasa kwa bahati nzuri tuna mechi ambazo angalau unaweza kuziita nyepesi mpaka pale tutakapokutana na 'The inform Gunners'  Arsenal November 10. Lakini angalau hizi mechi na timu ndogo tusifanye makosa au Moyes ajiandae kutuletea aibu ya kukosa ubingwa na kukosa hata kushiriki Champions League msimu unaokuja.

No comments:

Post a Comment