Wednesday 25 September 2013

SABABU YA PAOLO DI CANIO: KUFUKUZWA SUNDERLAND

by rahim kassonga



NI BAADA YA MECHI 13 NA SUNDERLAND TU!!

Sunderland wamemtimua Meneja wao Paolo Di Canio baada ya mwanzo mbovu kwenye Ligi Kuu England ambapo Timu hiyo imejikuta ipo mkiani kwenye Msimamo wa Ligi hiyo.
Tangu ateuliwe kuwa Meneja wa Sunderland Mwezi Machi, Di Canio, mwenye Miaka 45, ameshinda Mechi 3 tu kati ya 13 alizosimamia na Msimu huu ameambua Pointi 1 tu katika Mechi 5 za Ligi.
Klabu ya Sunderland imetoa tamko kuwa mrithi wa Di Canio atatangazwa hivi karibuni na kwa sasa Timu hiyo itakuwa chini ya Kocha Kevin Ball.
WASIFU WA PAOLO DI CANIO:
-KUZALIWA:
Rome, 9 Julai 1968
-KLABU ALIZOCHEZA:
Lazio, Juventus, Napoli, AC Milan, Cisco Roma, Celtic, Sheffield Wednesday, West Ham, Charlton
-FAINI:
£10,000 Mwaka 1998 kwa kumsukuma na kumwangusha Refa Paul Alcock baada ya kutolewa katika Mechi dhidi ya Arsenal
-TUZO YAUCHEZAJI WA HAKI:
Mwaka 2001 kwa kudaka Mpira badala ya kufunga ili Kipa wa Everton Paul Gerrard apate Huduma ya Kwanza baada ya kuumia.
-APONDWA:
Mwaka 2005 kwa kutoa Saluti ya Kifashisti kwenye Gemu na Lazio.
-ATEULIWA:
Bosi wa Swindon Mei 2011 na kuwapandisha LIGI 1 Mwaka mmoja baadae
-AJIUZULU:
Kama Bosi wa Swindon Februari 2013
-AMBADILI:
Martin O'Neill kama Meneja wa Sunderland Machi2013 na kuinusuru kushushwa Daraja toka Ligi Kuu England.
-ATIMULIWA:
Sunderland baada Mechi 5 za Ligi ambazo amefungwa 4 kati ya hizo na Sare moja.
Mechi ya kwanza chini ya Kocha Kevin Ball itakuwa ni leo watakapocheza Nyumbani Stadium of Light na Peterborough United kwenye Raundi ya Tatu ya Capital One Cup.
Baada ya Mechi hiyo, Sunderland watakuwa Wenyeji kwa Liverpool Jumapili ijayo, kisha kucheza na  Manchester United Oktoba 5 na kufuatia Dabi ya eneo la Wear-Tyne dhidi ya Newcastle hapo Oktoba 27.
Mwezi Machi Mwaka huu, Di Canio alitinga Sunderland kuchukua nafasi ya Martin O'Neill, aliefukuzwa na akakaribishwa na madai kuwa yeye anasapoti Mafashisti.
Meneja huyo kutoka Italy mwenye vituko amekuwa mwepesi kuwaponda Wachezaji wake waziwazi Magazetini na hili limeleta mkwaruzo ndani ya Timu.
Mbali ya kusaini Wachezaji 14 kwa ajili ya Msimu huu mpya, Di Canio pia aliwauza Wachezaji mahiri Kama Kipa Simon Mignolet kwa Liverpool na Stephane Sessegnon kwa West Brom ambae hivi Juzi katika Mechi yake kwanza tu na West Brom alifunga Bao walipoicharaza Sunderland 3-0.
Sunderland sasa inasaka Meneja mpya wa 6 katika kipindi cha chini ya Miaka mitano.
HABARI toka ndani ya Sunderland zimesema kuwa Wachezaji Wakongwe wa Klabu hiyo walimkabili Mkurugenzi Mtendaji Margaret Byrne na kulalamika kuhusu Paolo Di Canio kabla hajafukuzwa kama Meneja wao.
Mara baada ya kufungwa na West Brom 3-0 hapo Jumamosi, Siku ya Pili Di Canio alifanyiwa Mkutano na Wachezaji ambao unadaiwa cheche ziliwaka.


Baadae ndio Kundi hilo la Wachezaji Wakongwe likamfuata Mkurugenzi Mtendaji na kumwambia kuwa Mtaliana huyo hawezi kubaki kwani himaya yake ni ya Kikatili na mbovu kwa kuwaponda Wachezaji hadharani.
Miongoni mwa wanaotajwa kuchukua nafasi hiyo ni Meneja wa zamani wa Chelsea Roberto Di Matteo na wengine ni Gus Poyet, Tony Pulis na Alex McLeish.
Wakati huohuo
Meneja wa sasa wa Hull City - Steve Bruce amedai kuwa Paolo Di Canio staili yake ya uongozi ndio imemfukuzisha kazi ya Umeneja huko Sunderland.
Inaaminika staili ya Di Canio ya kuwa mkali na kuwaponda Wachezaji wake hadharani ilileta manung’uniko miongoni mwa Wachezaji na ni sababu kubwa iliyomfanya afukuzwe.
Steve Bruce, ambae aliwahi kuwa Meneja wa Sunderland kati ya Mwaka 2009 na 2011, amesema: “Huwezi kuwa Meneja wa Klabu ya Ligi Kuu siku hizi huku ukiongoza kwa kutisha Watu. Kuongoza Watu vizuri ni muhimu kuliko hata kufundisha Soka. Ukiwa Ligi Kuu Wachezaji wote ni wazuri na kilichobaki ni kuwafanya wacheze vizuri zaidi. Huwezi kuongoza kwa kuponda Watu hadharani. Namwonea huruma. Meneja amepoteza kazi. Utawala ni kazi ya upweke na amepoteza kazi. Nimewahi kupitia hilo na si kitu kizuri”
 

No comments:

Post a Comment