FOWADI
wa Arsenal Theo Walcott atakuwa nje ya Uwanja kwa Wiki kadhaa kwani Jumatano
anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa Tumbo huko Ujerumani ili kutibu matatizo ya
majeruhi aliyopata kwa ndani.
Akithibitisha
habari hizi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amekiri kuwa Walcott atakuwa nje
kwa Wiki kadhaa.
Matatizo
haya yatamfanya Mchezaji huyo azikose Mechi mbili muhimu za mwisho za England
za kuwania kufuzu kwenda Brazil Mwakani kwenye Fainali za Kombe la Dunia ambazo
wanatakiwa washinde ili wajihakikishie kufuzu.
England
watacheza na Montenegro Hapo Oktoba 11 na kumalizia Mechi ya mwisho ya Kundi
lake na Poland hapo Oktoba 15 na Mechi zote hizo zitachezwa Wembley Jijini
London.
Walcoot
alishawahi kupata matatizo ya aina hii Mwezi Machi na kuwa nje ya Uwanja kwa
Wiki 3.
Hata
hivyo, Wenger amehakikisha kuwa tatizo la Walcott sio kubwa sana na muda mfupi
baada ya Operesheni yake ataanza tena Mazoezi mepesi.
No comments:
Post a Comment