Monday 22 September 2014

CHADEMA kuanza maandamano Leo licha ya kupigwa marufuku


Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA kinatarajia kuanza maandamano hii leo ya kushinikiza bunge la katiba linaloendelea mjini Dodoma  lisitishwe ili kuacha kufuja fedha ambazo ni kodi ya wananchi.
Hayo yamebainishwa jana  na Mkurugenzi wa oganaizesheni  na mafunzo ya kanda wa chama hicho,  Benson Kigaila wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mchakato mzima wa katiba mpya.
Benson amesema takribani shilingi bilioni  47 zinatarajiwa kutumika katika bunge hilo la katiba ambazo kama zingetumika kwenye shughuli za  maendeleo,  nchi ingeweza kukua kiuchumi kwa hatua fulani.
Hata hivyo Jeshi la polisi limekwishatangaza kupiga marufuku maandamano hayo

No comments:

Post a Comment