Wednesday 24 September 2014

Sababu za Madee kushikiliwa na Polisi.. chanzo ni hiki cha jamaa wawili wa Pikipiki


jps
Taarifa zimethibitishwa kuhusu staa wa hit single kama ‘pombe yangu’ ‘tema mate tuwachape’ na ‘ni shidaah’ Madee ambae ni msanii kutoka kundi la TipTop Connection kushikiliwa na Polisi.

Kabla ya kuongea na meneja wa kundi hilo ambae ni Babtale, CHANZO kilisema ‘inasemekana Jumamosi iliyopita Madee aliporwa simu yake na watu wawili usiku huko Kigamboni’
Babtale alipoulizwa akasema ‘Kwenye mida ya saa tisa usiku Madee wakati anatoka kwenye show Kigamboni kuna waporaji simu wakiwa kwenye pikipiki wakampora kwa hiyo ikabidi gari aliyokuwemo Madee ikiendeshwa na Kwebe ianze kuikimbiza ile pikipiki alafu wakaigonga pikipiki kwa nyuma, pikipiki ilivyodondoka yule aliekua nyuma kwenye pikipiki ambae ndio alipora simu akafanikiwa kukimbia hivyo wakaishia tu kumkamata aliekua anaendesha hiyo pikipiki’
Madee 1
‘Wakamchukua na kwenda nae maskani Tiptop… mama yake akaja akasema msipeleke Polisi mwekeni hapa mi nakwenda kuwachukulia vitu vyenu, Madee kwa sababu alikua anakwenda kwenye show Mwanza ikabidi aende zake…… saa nne asubuhi yule mama akaja na Polisi badala ya kuja na mwizi mwenzake akaja na Polisi kataka kuwaokota watoto wote ofisini kwangu pale Tiptop, walimchukua huyo Muhalifu kwenye Land rover mpaka Polisi Magomeni na kubadilisha kibao kwamba huyu mtuhumiwa alitekwa’

‘Alipigwa akaumia hivyo wakamuombea PF3 wakampeleka Hospitali, nikapigiwa simu na Madee kwamba anatakiwa Polisi akaripoti…. kufika kituoni wakakuta ile pikipiki na kukuta yule dogo ndio anafika kutoka Hospitali akawaambia huyu ni mwizi ameiba, ikabidi Dogo aingizwe ndani jana akalala pale Polisi Magomeni’
note 3
‘Asubuhi yake Madee akaenda kituoni kama kufata Mwalifu wake na kutaka simu yake aliyoibiwa, akaambiwa kesi inabidi ihamishiwe Kigamboni…. saa kumi na mbili jioni ndio Kwebe ananitumia msg anasema Madee analalamika mbona humfatilii nikauliza kuna nini tena akasema wamemuingiza ndani, nikapiga simu Polisi Kigamboni ndio wakaniambia kijana wako tulitaka kumtoa lakini hatuwezi sababu amemteka mtu, nikapiga simu kwenye vyanzo vyangu vya msaada tukamtolea dhamana…. ni hilo, yataisha kama yalivyoanza’

No comments:

Post a Comment