Sunday 28 September 2014

RAMSEY, WILSHERE NA ARTETA WOTE NJE WIKI AU ZAIDI ARSENAL BAADA YA KUUMIA JANA DHIDI YA SPURS


Kiungo wa Arsenal, Aaron Ramsey akitolewa nje jana baada ya kuumia dhidi ya Spurs
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha Aaron Ramsey, Jack Wilshere na Mikel Arteta wote watakuwa nje wiki ijayo- maana yake majeruhi hao wataukosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray Jumatani. 

watatu hao wote wanatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Chelsea Jumapili ijayo, baada ya kuumia jana katika sare ya 1-1 na Tottenham Hotspur Uwanja wa Emirates.
Wenger amesema: "Sifahamua muda mrefu kiasi watakuwa nje, lakini watakosekana wiki ijayo. Nafikiri Ramsey ni nyama (maumivu), na Arteta ni misuli ya nyuma ya mguu. Wilshere ni kifundo cha mguu,"amesema.

No comments:

Post a Comment