Wednesday 24 September 2014

UFUNGUZI WA WARSHA YA KUJENGA UELEWA WA WADAU KUHUSU MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI – TASAF AWAMU YA TATU MKOANI KATAVI


 Meneja Uratibu kutoka TASAF Makao Makuu Tunu Munthali (aliyesimama) akiwasilisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe (wa kwanza kulia) salaam za Mkurugenzi mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga.  

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dkt. Rajabu Rutengwe akihutubia washiriki wa Warsha ya kujenga uelewa wa wadau kuhusu mpango wa kunusuru Kaya maskini – TASAF awamu ya tatu Mkoani Katavi . 
Hawa nao ni sehemu ya washiriki wa warsha hiyo inayoshirikisha watendaji mbalimbali wa ngazi ya Mkoa, Wilaya, Tarafa na Kata wakifuatilia kwa makini maelezo ya ufunguzi toka kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe (hayupo pichani) Baadhi ya washiriki wa Warsha hiyo wakimsikiliza hotuba ya ufunguzi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe  (hayupo pichani)  Picha hii na zingine zilizopo chini yake ni za picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Rutengwe (wa tatu kwa waliokaa) na makundi mbalimbali ya washiriki wa warsha  ya kujenga uelewa wa wadau kuhusu mpango wa kunusuru Kaya maskini – TASAF awamu ya tatu Mkoani Katavi, wengine waliokaa kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Bw. Seleman Lukanga, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bw. Paza Mwamlima na Meneja uratibu TASAF Tunu Alice Munthali. Wengine ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda Enock Gwambasa na Makamu M/Kiti Yusuf Msengi Ngassa

No comments:

Post a Comment