Tuesday 23 September 2014

PINDA AHUDHURI IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU MWAIPOPO WA DAYOSISI YA SUMBAWANGA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika ibada ya kumweka wakfu Askofu wa  Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo katika Kanisa kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga Septemba 11, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu (kushoto) wakiwa katika Picha ya pamoja na Askofu wa  Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo  na mkewe Tunsume Mwaipopo (kulia) katika katika ibada ya kumsimika Askofu huyo iliyofanyika  kwenye  Kanisa kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga Septemba 11, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda   na mkewe Tunu  (wapili kulia) wakimkabidhi  zawadi Askofu wa Dayosisi ya  Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo (wapili kushoto) katika ibada ya kumweka wakfu Askofu huyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Kiinjili la Kilutheri mjini Sumbawanga, Septemba 21, 2014. Kulia ni mke wa Askofu huyo, Tunsume Mwaipopo  na kushoto ni Askofu Israel Mwakyolile wa Dayosisi ya Konde.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda   na  mkewe Tunu (wapili kulia)  wakisalimiana na Askofu Damian Kyaruzi wa Jimbo la Sumbawanga (kulia) katika Ibada ya kumweka wakfu Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Ambele Mwaipopo iliyofanyika kwenye kanisa kuu la kiinjili la Kilutheri la mjini Sumbawanga Septemba 21, 2014. Wapili kushoto ni Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Alex Malasusa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment